logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Rachael Aeleza Kwa Nini Ataishi Daima Na Pete Ya Otuoma Ya Ndoa Kidoleni Mwake

“Otuoma ataishi kwa moyo wangu milele. Huyu mwanamke hapa (akiashiria kwenye jeneza) alinipenda kwa roho yake yote, alinipa heshima kama mwanamke na kila kitu nilihitaji angenipa.”

image
na MOSES SAGWEjournalist

Burudani12 January 2025 - 09:02

Muhtasari


    TIKTOKER Rachel Otuoma aliwapunga wengi kwa hotuba yake yenye ukakamavu wa kipekee wakati wa mazishi ya mume wake, mwanasoka Ezekiel Otuoma.


    Mrembo huyo ambaye aliganda na mumewe licha ya hali yake ya ugonjwa wa kupooza neva mwilini kwa takribani miaka minne, alisema kwamba hana mpango wa kuasi kiapo chake cha ndoa.


    “Vile tulikutana tukapendana, mapenzi hayakuwahi isha. Na mumeona vile nilikula kiapo cha kuwa naye kwa hali mbaya na nzuri, hata mzee mwenyewe alisema ni kipo itatutenganisha,” Rachael alianza.


    “Hivyo, ilikuwa ni ‘for better, for worse’ na sisi tulikuwa kwa hiyo ‘worse’ kwa miaka 4 tulikuwa tunaingia mwaka wa 5,” Rachael aliongeza.


    Alisema kwamba hali ya ugonjwa wa Otuoma haikuwa rahisi lakini kadri muda ulivyozidi kusonga, aliikubali hali hiyo, akisisitiza kwamba hatokuja kumsahau mwanasoka huyo katika maisha yake.


    Rachael alionyesha waombolezaji pete yake ya ndoa na Otuoma na kufichua kwamba haitowahi kutoka katika kidole chake katika maisha yake yote.


    “Otuoma alipatikana na ugonjwa wa Motor Neurone, na hiyo safari ya kushughulikia mgonjwa wa huo ugonjwa sio rahisi. Inahitaji mtu ako na utu, kujitolea ama heshima yako kama mwanamke.”


    “Kwa kweli nili’heal na hali ya Otuoma, kwa sababu huyu ni mtu nilipenda na bado nampenda nap eye yake ndio hii nievaa, niko na pete mbili sasa. Haitawahi nitoka kwa mkono wangu,” Rachel alisema huku akiwaonyesha waombolezaji pete hiyo kidoleni.


    Akifunguka kwa nini ameamua kuchukua uamuzi huo licha ya kutofanikiwa na mtoto na Otuoma, Rachel alisema kwamba mwanasoka huyo alikuwa mtu mwenye mapenzi ya dhati kwake aliyempa heshima yake kama mwanamke.


    “Otuoma ataishi kwa moyo wangu milele. Huyu mwanamke hapa (akiashiria kwenye jeneza) alinipenda kwa roho yake yote, alinipa heshima kama mwanamke na kila kitu nilihitaji angenipa,” alisema.


    “Hata kitu chochote mama yangu angetaka, huyu mwanamume angempa na hiyo ndio sababu nilimpa Otuoma heshima inayomfaa,” aliongeza huku akifichua kwamba huu ungekuwa maka wao wa 10 kwenye kumbukumbu ya ndoa.



    RADIO JAMBO FREQUENCIES

    Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


    logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved