logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Vera Sidika Na Huddah Monroe Waotesha Upya Bifu Lao Mitandaoni

Tamko la Monroe linajiri wiki moja baada ya Netflix kuachia msimu wa tatu wa Young, Famous and African, shoo ya kiuhalisia ambayo inawahusisha mastaa katika sanaa ya burudani barani Afrika.

image
na MOSES SAGWEjournalist

Burudani24 January 2025 - 09:51

Muhtasari


  • Usemi huu ulioonekana kudunisha shoo za kiuhalisia uliamusha popo za Vera Sidika ambaye amehusika katika shoo nyingi za kiuhalisia, ya hivi karibuni ikiwa ile ya Real Housewives of Nairobi.



WANASOSHOLAITI Vera Sidika na Huddah Monroe wameanzisha upya bifu lao kwenye mitandao ya kijamii kisa kuhusika katika uigizaji wa filamu za kihalisia.


Zogo hilo lilianza pale Huddah Monroe alipotoa maoni yake kuhusu wanasosholaiti kuigiza katika shoo za kiuhalisia kwenye runinga.


Mfanyibiashara huyo wa bidhaa za urembo aliashiria kwamba yeye hawezi kuigiza kwenye filamu hizo za kiuhalisia kwani kulingana na yeye, shoo hizo haziongezi chochote cha mno katika maisha ya mtu zaidi ya maigizo tu ya maisha feki.


“Ni afadhali nitazame video za mbwa na paka kuliko kutazama shoo ya kiuhalisia au simulizi ya maisha ya mtu kwenye vlog ya YouTube. Siwezi hata jitazama mimi mwenyewe. Mkiwa wakweli, baada ya kutazama hizi shoo zote za uhalisia, ni vipi ziliboresha maisha yenu? Kuna kitu mlijifunza? Zilikuwa na athari yoyote katika maisha yenu?” Huddah alihoji.


Usemi huu ulioonekana kudunisha shoo za kiuhalisia uliamusha popo za Vera Sidika ambaye amehusika katika shoo nyingi za kiuhalisia, ya hivi karibuni ikiwa ile ya Real Housewives of Nairobi.


Sidika alicharuka kwenye Instagram na kumzomea vikali Huddah Monroe ambapo alidai kwamba mwanasosholaiti huyo mwenzake huenda anachukia shoo za kiuhalisia baada ya kukataliwa kuhusika katika moja miaka ya nyuma.


“Jinsi mtu Fulani anavyojitokeza akidai kuchukua shoo za kiuhalisia wakati alihusika katika moja miaka 10 iliyopita ni ushetani. Ooh na alifukuzwa siku 5 baadae kwa kufanya kazi duni. Kuhukumu watu kwa kutazama shoo za kiuhalisia si ukichaa huo? Wakati ulikuwa kwenye moja ambayo ilikuendea mrama, hebu ifanye ieleweke,” Vera Sidika alijibu mipigo.


Sidika aliendeleza manung’uniko yake kwa Huddah Monroe akimshauri kwamba kama aliwahi kuhusika katika shoo ya kiuhalisia, hafai kuwa hakimu kuwaamulia watu kama wanastahili kutazama au la.


‘Kama umewahi kuhusika katika shoo ya kiuhalisia hufai kuwa mmoja wa kuwahukumu watu kwa kuitazama. Wewe kunywa tu maji na ujishughulishe na mambo yako, haswa wakati unajua kwamba ilikuendea kombo,” Sidika aliongeza.


 


Tamko la Monroe linajiri wiki moja baada ya Netflix kuachia msimu wa tatu wa Young, Famous and African, shoo ya kiuhalisia ambayo inawahusisha mastaa katika sanaa ya burudani barani Afrika.


 



RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved