logo

NOW ON AIR

Listen in Live

“Miaka 10 Iliyopita, Shetani Alifanikiwa Kuniondoa Kanisani” – Vera Sidika

“Ni mpaka miaka kumi iliyopita wakati shetani alifanikiwa kuniondoa kanisani lakini mimi ni Mkristo 1000%. Ni vile tu sijakuwa nikienda kanisani kwa muda sasa."

image
na MOSES SAGWEjournalist

Burudani28 January 2025 - 09:55

Muhtasari


  • “Nilifikiria wewe ni Muislamu Vera,” shabiki alimuuliza.
  • “Ulisikia wapi? Maisha yangu yamekuwa ya kanisani tangu siku za Sunday School,” Vera Sidika alisema.



MWANASOSHOLAITI Vera Sidika amefichua kwamba yeye hata siku moja hujawahi badili dini kutoka Ukristo kwenda Uislamu.


Sidika alifichua haya kwa shabiki mmoja ambaye alistaajabu kwamba kwa muda wote amekuwa akifikiria kwamba Sidika ni Muislamu.


“Nilifikiria wewe ni Muislamu Vera,” shabiki alimuuliza.


Vera alimjibu akisema kwamba maisha yake yote tangu utotoni yamejikita katika Ukristo na kufichua kuwa alianza kuenda kanisani tangu enzi za mafunzo ya watoto Jumapili kanisani.


“Ulisikia wapi? Maisha yangu yamekuwa ya kanisani tangu siku za Sunday School,” Vera Sidika alisema.


Hata hivyo, alifichua kwamba miaka kumi iliyopita, shetani alimrubuni na kufanikiwa kuondoka maisha yake katika mkondo wa kanisani lakini pia akafichua kuwa katika siku za hivi karibuni amekuwa akipiga hatua za kipekee katika kuyarudisha maisha yake kanisani.


“Ni mpaka miaka kumi iliyopita wakati shetani alifanikiwa kuniondoa kanisani lakini mimi ni Mkristo 1000%. Ni vile tu sijakuwa nikienda kanisani kwa muda sasa japo katika siku za hivi karibuni nimekuwa nikifanya juhudi za kurekebisha uhusiano wangu na Mungu,’ alisema.


Hii si mara ya kwanza kwa mama huyo wa watoto wawili kuzungumzia kuhusu maisha yake na jinsi alipotoka kutoka njia ya kuenda kanisani.


Mapema mwaka jana, Sidika aliomba mashabiki wake ushauri wa kanisa ambalo lingemfaa kwa ibada za kila Jumapili, akidokeza kwamba alikuwa na nia ya kumrudia Mungu.


Mwaka huu wa 2024 ninataka kujenga uhusiano mwema na Mungu, sijawahi kuenda kanisani kwa muda sasa, mimi ni muumini, namuomba Mungu na kufanya upande wangu kama Mkristo. Lakini inniwia vigumu kwenda kanisani. Watu wananiangalia sana. Kunaye mmoja wenu ambaye anajua kanisa zuri ambalo sitoweza kusumbuliwa na kuangaliwa, tafadhali pendekeza moja,” Vera Sidika aliomba.


Mwishoni mwa 2024, Sidika alichapisha video akiwa kanisani na kuonyesha furaha yake kumaliza mwaka kwa kutimiza ahadi yake ya kuanza kumsaka Mungu.


“Jumapili hii iliyopita ilikuwa mara yangu ya kwanza kanisani kwa zaidi ya miaka 10 shukrani kwa BFF wangu @dyna_muthoni. Ilikuwa azimio yangu ya mwaka mpya lakini shetani aliijaribu kwa miezi 10. Kila mara ‘nilisema nitaanza Jumapili hii’ haikuwahi kutokea. King’s house ni kanisa nzuri kweli,” aliandika.



RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved