logo

NOW ON AIR

Listen in Live

“Rudini Kwa Gospel Mpate Huruma”Weezdom Asuta Kolabo Za Bahati Na Pozee

“Watu watafute watu wa kuandika ngoma kusema kweli, ama mrudi kwa injili yetu hapa angalau huku kuna huruma mtahurumiwa,” Weezdom aliwaasa.

image
na MOSES SAGWEjournalist

Burudani01 February 2025 - 14:06

Muhtasari


  • Msanii huyo alidai kwamba msanii yeyote ambaye hakuchukua fursa ya kufaidika kutokana na ugomvi wake na Willy Paul basi atakufa maskini kwani bifu lenyewe tayari limefika mwisho.



ALIYEKUWA msanii wa lebo ya Bahati, EMB Records, Weezdom amekuwa mtu wa kwanza kukosoa vikali kolabo mbili za Bahati na Willy Paul zilizoachiliwa Ijumaa Januari 31.


Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Weezdom alidai kwamba kolabo hizo mbili – Keki na Paah, hazikuwa na ubora wowote licha ya Bahati na Willy Paul kuzipigia debe pakubwa.


Weezdom alisema kwamba alijutia kutumia muda wake kusikiliza tungo za wawili hao ambao waliondoka katika fani ya miziki ya Injili, akiwataka warudi kwenye injili.


Msanii huyo ambaye pia alionekana kupotoka kutoka kwa injili kuwafuata wawili hao aliashiria kwamba yeye bado ni msanii wa injili na kusema yuko tayari kuwakaribisha wawili hao watakapofikia uamuzi wa kurudi.


Kwa mujibu wa Weezdom, Bahati na Willy Paul wakirudi kwa fani ya miziki ya injili angalau wataonewa huruma, akidai kwamba fani ya miziki ya kidunia imewakataa na ngoma zao haziwezi onewa huruma hata chembe.


“Ni nini hiki ambacho nimekisikiliza? Wuueh, kusema ukweli kila mtu ako na maskio yake. Lakini aai, hapo hakuna kitu. Watu watafute watu wa kuandika ngoma kusema kweli, ama mrudi kwa injili yetu hapa angalau huku kuna huruma mtahurumiwa,” Weezdom aliwaasa.


Kuelekea muda wa kuachiliwa kwa kolabo hizo, Bahati alidai kwamba hii ni enzi mpya ambayo yeye na Pozee wameanza, akisema kwamba wamekuwa wakitawala muziki wa Kenya kwa miaka 10 iliyopita na sasa hawako tayari kuondoka.


Msanii huyo alidai kwamba msanii yeyote ambaye hakuchukua fursa ya kufaidika kutokana na ugomvi wake na Willy Paul basi atakufa maskini kwani bifu lenyewe tayari limefika mwisho.


“Unajua sasa hivi ndio tumeanza, ni enzi mpya na ujue bado sisi ndio tumekuwa tukishikilia kwa miaka 10 na ndio tunaanza tena. Hivyo kama kuna msanii hakutengeneza pesa huo wakati ajue sasa atakufa maskini maana sisi tumerudi,” Bahati alisema huku Willy Paul akimuunga mkono kwamba hii ni enzi ya kuwafuuza wasanii wa kigeni kutoka kilele cha chati za muziki humu nchini.



RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved