logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Director Trevor Akemea Vikali Video Ya Bradley Mtall Akicheza Na Simba Jike Dubai

Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Trevor alikashifu video inayomuonyesha Bradley akishrutishwa kucheza karibu na simba jike.

image
na MOSES SAGWEjournalist

Burudani02 February 2025 - 12:09

Muhtasari


  • Trevor aliwataka Gen Goliath na Zam Zam kwa Pamoja kuondoa mara moja video hiyo ambayo imekuwa gumzo kwenye mtandao wa TikTok.
  • Trevor pia alibainisha kwamba video hizo zinachapishwa bila uhakiki kutoka upande wake kama meneja.



MENEJA wa Bradey Mtall maarufu kama Gen Z Goliath, Director Trevor ametoa kauli yake kuhusu video inayopiga misele kwenye mitandao ya kijamii ya jamaa huyo wakati wa ziara yake jijini Dubai, UAE.


Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Trevor alikashifu video inayomuonyesha Bradley akishrutishwa kucheza karibu na simba jike.


Bradley Mtall amekuwa Dubai kwa wiki moja, shukrani kwa kampuni ya Zam Zam ambayo inajishughulisha na uuzaji wa bidhaa za kielektroniki haswa simu za iPhone.


Trevor ambaye hivi majuzi ameweka wazi kwamba Bradley alipata meneja mpya wa kusimamia shughuli zake zingine na kumuacha Trevor kama meneja mbadala, hata hivyo aliwashukuru Zam Zam kwa kile wanachomfanyia Bradley.


Trevor alisema kwamba licha ya Zam Zam kumsaidia Bradley, haifai kabisa kumshurutisha kucheza karibu na mnyama mwitu hatari kama simba hata kama amefungwa.


“Nimekutana na video inayoenea ya Goliath na Zam Zam, na ningependa kuchukua muda kidogo kukashifu vikali maudhui kama yale. Wakati ninahongera sana juhudi za Zam Zam kumpa sapoti Gen Z Goliath wetu, ni vizuri kuelewa kwamba ubunifu una mipaka yake,” Trevor alianza.


Trevor aliwataka Gen Goliath na Zam Zam kwa Pamoja kuondoa mara moja video hiyo ambayo imekuwa gumzo kwenye mtandao wa TikTok.


Trevor pia alibainisha kwamba video hizo zinachapishwa bila uhakiki kutoka upande wake kama meneja.


“Ningependa kwa heshima kubwa kuwauliza wafute video hiyo ya TikTok ambayo imekuwa ikipiga misele mitandaoni. Pia ningependa Wakenya wajue kwamba video hizi zinachapishwa bila sisi kuidhinisha kwa sababu hatuna haki kwazo.”


“Mwishow a siku, utengenezaji wa maudhui ni safari ya kujifunza. Wakati mwingine, tunafanya makosa bila kugundua, lakini cha muhimu ni kwamba tunatambua makosa hayo na kujifunza kutokana nayo. Ningependa kuwajulisha kwamba makosa kama hayo hayatatokea tena mbeleni,” Trevor alisema.


Video ya Bradley Mtall akicheza na simba jike jijini Dubai imekuwa ikisutwa na wengi, baadhi hata wakizua utani kwamba simba huyo akifanya makosa kumpararua kijana huyo basi wote watajitokeza na kufurika jijini Dubai wakitaka haki kutendeka.


 



RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved