logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Willy Paul Adai Video Ya Kolabo Ya‘Keki’ Na Bahati Ilimgharimu Ksh3.5M

“Nilitumia taslimu ya Shilingi milioni 3.5 kwenye video hii na ndugu yangu Bahati. Bahati sasa yuko kwenye mikono salama,” Willy Paul aliandika.

image
na MOSES SAGWEjournalist

Burudani02 February 2025 - 12:38

Muhtasari


  • “Nilitumia taslimu ya Shilingi milioni 3.5 kwenye video hii na ndugu yangu Bahati. Bahati sasa yuko kwenye mikono salama,” Willy Paul aliandika.
  • Bahati alifika kwenye chapisho hilo na kumtania Willy Paul akimtaja kama “msanii Tajiri”.



SIKU moja baada ya kuachia kolabo zao mbili, Willy Paul na Bahati sasa wamedadavua kiasi cha pesa ambacho video ya ngoma moja – Keki, iligharimu.


Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Willy Paul alifichua kwamba video ya ngoma hiyo ambayo imewavutia wengi chini ya saa 24 baada ya kuiachia ilimgharimu Zaidi ya shilingi milioni 3 pesa za Kenya.


“Nilitumia taslimu ya Shilingi milioni 3.5 kwenye video hii na ndugu yangu Bahati. Bahati sasa yuko kwenye mikono salama,” Willy Paul aliandika.


Bahati alifika kwenye chapisho hilo na kumtania Willy Paul akimtaja kama “msanii Tajiri”.


Hata hivyo, licha ya ngoma zao kuwavutia wengi, baadhi wanahisi kwamba hazijafika viwango ambavyo wengi walitarajia.


Mmoja wa wanaokosoa ngoma hizo ni msanii Weezdom ambaye alidai kwamba hazina ubora wowote akionekana kujuta kuyapa masikio yake nafasi ya kuzisikiliza.


Kwa mujibu wa Weezdom, Wawili hao wanastahili kutafuta watu wa kuwatungia nyimbo wao wasalie tu katika kuimba, akikashifu utunzi wao.


Weezdom aliwasuta akiwataka kufanya hima kurudi katika Sanaa ya injili, akidai kwamba huko angalau wataonewa huruma.


“Ni nini hiki ambacho nimekisikiliza? Wuueh, kusema ukweli kila mtu ako na maskio yake. Lakini aai, hapo hakuna kitu. Watu watafute watu wa kuandika ngoma kusema kweli, ama mrudi kwa injili yetu hapa angalau huku kuna huruma mtahurumiwa,” Weezdom aliwarai.


Itakumbukwa kwamba Weezdom ni msanii aliyechipukia kimuziki shukrani kwa Bahati na lebo yake ya EMB Records.


Hata hivyo baada ya Bahati kuhamia miziki ya kidunia, ukuruba wake na Weezdom ulionekana kuzorota ambapo msanii huyo amekuwa akimzomea hadharani mitandaoni bosi wake wa zamani.


Mwaka jana pia Weezdom alimkasifu Willy Paul kwa kile alidai kwamba alikataa kujitokeza kumpa msaada wakati alikuwa amelazwa hospitalini.


Weezdom alifichua kuzuiliwa katika hospitali moja kwa Zaidi ya miezi 3 katika kile alichodai kwamba ni kukosa bili ya matibabu.


Alirudi kwa mashabiki wake wa mitandaoni na baada ya kufanikiwa kutoka, alisema kwamba illy Paul alifumbia jicho suala lake la uhitaji wa msaada kulipia matibabu yake.



RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved