logo

NOW ON AIR

Listen in Live

‘Nitazalisha Mwingine Hawa Wakinipa Stress!’ Jamaa Mwenye Babymamas 7 Asema

Alisema kwamba yeye hupata tulizo la moyo katika kumpa mwanamke mimba pindi anapohisi kuwa na msongo wa mawazo kutokana na mahusiano na wanawake wengine.

image
na MOSES SAGWEjournalist

Burudani20 February 2025 - 09:48

Muhtasari


  • Wengine pia walimkosoa kwa kurasmisha uchepukaji katika ndoa kuonekana kama jambo la kawaida licha ya kuwepo kwa magonjwa ya zinaa mengi.
  • @Victoria Anene: Unaweza kufikiria. Mwanaume huyu anadhani anawafanyia wanawake upendeleo.

mwanamume mwenye babymamas 7

MWANAMUME ambaye anajipiga kifua kwa kuwa na familia pana yenye wake halali wawili na wanawake wengine 5 ambao amezalisha nje ya ndoa amedai kwamba yuko tayari kuendeleza msururu wake wa kuzalisha wanawake tofauti tofauti.

Mwanamume huyo mwenye umri wa makamo alikiri hayo wakati alipotokea kwenye mahojiano ya runinga.

Alisema kwamba yeye hupata tulizo la moyo katika kumpa mwanamke mimba pindi anapohisi kuwa na msongo wa mawazo kutokana na mahusiano na wanawake wengine.

“Mimi nina wanawake wawili, pia nimezaa nje na wanawake 5 hivyo kwa jumla nina watoto 7 kutoka kwa wanawake 7. Na katika hawa wanawake wangu wawili, mmoja ni mzungu mwingine ni mwafrika. Na wote tumeoana kwa njia halali kabisa kwa neema ya Mungu,” Mwanamume huyo alieleza kwa majigambo tumbi nzima.

“Sasa, sharti nambari moja katika nyumba yangu ni kwamba kama watanipa msongo wa mawazo kupita kiasi hiyo inamaanisha ni lazima nitoke nitafute mwanamke mwingine, kwa sababu naamini ninaishi mara moja tu!” aliongeza.

×

Video hiyo ambayo ilichapishwa kwenye ukurasa wa Facebook kwa jina 9ja Now ilivutia maoni mseto, baadhi wakimuunga mkono kwa dhana kwamba anafurahia maisha yake duniani huku wengine wakidai kwamba alikuwa anawachezea wanawake shere.

Wengine pia walimkosoa kwa kurasmisha uchepukaji katika ndoa kuonekana kama jambo la kawaida licha ya kuwepo kwa magonjwa ya zinaa mengi.

@Victoria Anene: Unaweza kufikiria. Mwanaume huyu anadhani anawafanyia wanawake upendeleo.

@Paul Mgbameh: Wewe ni mtu asiyewajibika sana.

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved