logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Mwanamuziki Gigy Money yuko tayari kuolewa kwa mwanaume yeyote

Mwanamuziki wa kike raia wa Tanzania Gift Stanford Joshua ambaye anajulikana kwa jina lake la usanii Gigy Money amefunguka kwamba anatamani ndoa kwa vyovyote vile.

image
na Japheth Nyongesa

Burudani21 February 2025 - 12:52

Muhtasari


  • Gigy Money pia aliwahi kudai kuwa na idadi kubwa ya utoaji mimba ila bado alifanikiwa kupata binti aliyempata na mpenzi wake wa zamani.
  • Mwanamziki huyo  mara kwa mara ametuhumiwa, kushtakiwa na wakati mwingine kupigwa marufuku kwa kukiuka utaratibu wa uendeshaji wa shughuli za sanaa nchini Tanzania.

Mwanamuziki wa kiker aia wa Tanzania  Gift Stanford Joshua ambaye anajulikana kwa jina lake la muziki Gigy Money amefunguka kwamba anatamani ndoa kwa vyovyote vile.

Kwa upande wake anasema yuko tayari kuingia katika ndoa bila kujali mahari atakayotoa mumewe. Pia anakiri kwamba anaamini sana kwenye mapenzi.

"Mimi niko na roho ngumu, mimi ata nikipata mwanaume muisilamu naolewa, yaani bora awe mwanaume, kama ng'ombe ndo tunakula tunakufa. Ata elfu moja. Mimi naamini kwenye mapenzi Hamisa sai amependa Azizi, watu wengi hawakwaamini hilo penzi liko. mimi naumia natamani ndoa yenye Penzi," mwanadada Money alieleza.

Mwanamke huyo Gigy Money aliwahi kudaiwa kuwa na uhusiano wa kimapenzi na mwanamuziki wa Tanzania Ali Kiba, ila Kiba kwa upande wake alikanusha madai hayo kutoka kwa vixen huyo.

Gigy Aliwahi kutoa kauli kwa umma kuhusu matamanio yake ya kupata watoto na mwimbaji maarufu wa bongo, rais wa Wasafi Diamond Platnumz na vilevile mtangazaji wa runinga ya Tanzania, Idris Sultan.

Mnamo mwaka 2020, Gigy Money alikuwa na mapigano makali  na mpenzi wake wa wakati huo ambaye alikuwa mzaliwa wa Nigeria kwa jina la utani Hunchy Huncho  ambao walitengana baada ya tukio hilo.

 Gigy Money pia aliwahi kudai kuwa na idadi kubwa ya utoaji mimba ila bado alifanikiwa kupata binti aliyempata na mpenzi wake wa zamani.

Mwanamziki huyo  mara kwa mara ametuhumiwa, kushtakiwa na wakati mwingine kupigwa marufuku kwa kukiuka utaratibu wa uendeshaji wa shughuli za sanaa nchini Tanzania.

Hili hasa limechangiwa pakubwa kwa kutumia lugha chafu na kuchapisha maudhui ya uchi kwenye mitandao yake ya kijamii.

Mwaka 2019 Baraza la Sanaa nchini Tanzania lilimpiga marufuku Gigy Money kufanya shughuli zozote za sanaa ndani na nje ya Tanzania kwa muda wa miezi sita na kutoa kiasi cha shilingi milioni moja za Kitanzania kwa kosa la kudhalilisha utu wake.

Aliadhibiwa, kisa alitumbuiza akiwa amevalia mavazi yaliyoonyesha mwili wake nusu uchi katika tamasha lililorushwa moja kwa moja kwenye runinga ya Wasafi ambayo pia ilipokea adhabu ya miezi sita kutoka kwa mamlaka ya Mawasiliano ya Tanzania kufuatia tukio hilo.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved