logo

NOW ON AIR

Listen in Live

“Bora 6:50am Impate Kwa Lami” Jamaa Ajitolea Kumpa Kairo Lift Kwenda Kazini Kila Siku

Kimani alisema kwamba Kairo ikiwa anahitaji hiyo ‘lift’ yake, basi itabidi anatokea kwa Barabara anayopita na gari lake alfajiri hiyo akimsubiri.

image
na MOSES SAGWEjournalist

Burudani22 February 2025 - 10:55

Muhtasari


  • Kimani alisema kwamba kwa vile Kairo kwa sasa yuko kwenye matatizo mengi, yeye kama rafiki yake amejitolea kumsaidia na ‘lift’ kila siku Kwenda kazini kwa kipindi cha miezi 3 ijayo. 
  • “Nina furaha kumpa kairo lifti kwenda kazini kwa miezi 3 ijayo bila malipo,Bora 6:50am ikue inampata kwa lami ameningojea,” Polo Kimani alisema.

Khalif Kairo

MTUMIZI mmoja wa mtandao wa X amejitolea kumsaidia muuzaji wa magari Khalif Kairo kwa usafiri katika kipindi cha miezi mitatu.


Polo Kimani, kupitia jukwaa la X alichapisha ujumbe akitoa ahadi hiyo kwa muuzaji huyo wa magari ambaye mwaka huu ulimuanzia vibaya biashara yake kuporomoka lakini pia kuwa mgeni wa vyombo vya dola mara kadhaa.


Kimani alisema kwamba kwa vile Kairo kwa sasa yuko kwenye matatizo mengi, yeye kama rafiki yake amejitolea kumsaidia na ‘lift’ kila siku Kwenda kazini kwa kipindi cha miezi 3 ijayo.


Hata hivyo, msaada wa Kimani hautakuja rahisi hivyo, alisema kwamba kama Kairo atahitaji kuaidiwa na ‘lift’ kila siku kwa miezi 3, asi sharti atii masharti yake ya kutokea kwa Barabara alfajiri ya saa moja kasoro dakika 10 kila siku ili kumsubiri amchukue.


Kimani alisema kwamba Kairo ikiwa anahitaji hiyo ‘lift’ yake, basi itabidi anatokea kwa Barabara anayopita na gari lake alfajiri hiyo akimsubiri.


“Nina furaha kumpa kairo lifti kwenda kazini kwa miezi 3 ijayo bila malipo,Bora 6:50am ikue inampata kwa lami ameningojea,” Polo Kimani alisema.

×

Aliendelea kumpa Kairo masharti zaidi akisema kwamba ni lazima akubali kuketi katika viti vya nyuma na bila kuongea chochote hadi afikishwe kazini kwake.


“Itabidi amekaa nyuma juu mbele ni kwa bibi,pia yeye nampeleka kazi,” Kimani aliongeza.


Hata hivyo, baadhi walimtania kwamba hiyo itakuwa ni kumkosea Kairo heshima ikizingatiwa kwamba mfanyibiashara huyo alikuwa mwenye Maisha ya kifahari mwaka jana.


Walimtania kwamba Kairo nim tu ambaye alikuwa amezoea Maisha ya gari la kifahari aina ya Porsche Cayenne na kwamba itamkalia vigumu kuabiri gari lolote lenye haiba chini ya Porsche.


Haya hapa baadhi ya maoni ya watumizi wa X kwenye chapisho hilo;


@wa_ngachu: Uko sure gari Yako itafika standards alikuwa ameset za Porsche cayenne kwanza Ile ya kupenda reggae music alafu ujue anapenda kutumia express way.


@snrgoodman: Huyu ni kijana wa cayenne mnapea ultimatum 😂😂😂


@nyuki6634: Kumbe pia wewe kairo alikusaidia ukanunuwa gari na huwa hamsemi 😂


 


 


 



RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved