logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Tweet Ya Zamani Mchuuzi Akitukana Msanii Zlatan Yamkosesha Msaada Wa 500k

Mchuuzi alivutia umakini wa mwimbaji na akachaguliwa kama mfadhili. Hata hivyo, kabla ya kutuma pesa hizo, Zlatan alipitia tweets zake za zamani na kugundua tweet ya 2020 ambapo alimkejeli.

image
na MOSES SAGWEjournalist

Burudani22 February 2025 - 15:28

Muhtasari


  • Mchuuzi alivutia umakini wa mwimbaji na akachaguliwa kama mfadhili. Hata hivyo, kabla ya kutuma pesa hizo, Zlatan alipitia tweets zake za zamani na kugundua tweet ya 2020 ambapo alimkejeli.
  • Tweet ya zamani ilikuwa jibu kwa chapisho la Zlatan ambapo alimuanika mtu mwenye ushawishi ambaye alikuwa na shida naye mnamo 2018.

Zlatan Ibile

MSANII wa Nigeria, Zlatan Ibile ameghairi nia yake ya kumkwamua kiuchumi mchuuzi wa kutembeza vyakula mitaani baada ya kugundua tweet ya mchuuzi huyo akimdhihaki kwa kejeli wakati akianza safari yake ya muziki.


Zlatan alikuwa radhi kabisa kumpa mchuuzi huyo msaada wa 500k kujikwamua kiuchumi baada ya kuhurumia hali yake, lakini kabla ya kumpa, alifanya upekuzi wa haraka kwenye Twitter (X) na kugundua mchuuzi huyo alikuwa mmoja kati ya watu waliokuwa wakikashifu muziki wake kipindi anajitafuta kutoboa kwenye tasnia ya Afrobeats.


Baada ya kuibua tweet hiyo ya 2020 mchuuzi huyo alikejeli muziki wake, Zlatan aliamua kusitisha msaada wake kwake na kumtaka kula ujeuri wake kwani ni mmoja kati ya wale ambao hawakuwahi amini kwamba angefanikiwa kimuziki.


Tukio hilo lilitokea baada ya Zlatan kutangaza zawadi kwenye jukwaa lake la X, na kuahidi N500K kila mmoja kusaidia wafanyabiashara wadogo ambao mara kwa mara hutangaza kazi zao mtandaoni.


Katika chapisho lake, Zlatan aliandika:


“Hii ni kwa ajili ya kujitolea na shauku—ikiwa umeshiriki kila mara au kutangaza kazi au bidhaa zako kwenye rekodi ya matukio yako, hii ni kwa ajili yako. Biashara yako ndogo inahitaji nini ili kustawi? Ninawezaje kukuunga mkono? Naenda kuangalia timeline yako kabla sijakutumia hela.” 

Zlatan Ibile akiahidi msaada kwa mchuuzi

Mchuuzi alivutia umakini wa mwimbaji na akachaguliwa kama mfadhili. Hata hivyo, kabla ya kutuma pesa hizo, Zlatan alipitia tweets zake za zamani na kugundua tweet ya 2020 ambapo alimkejeli.


Tweet ya zamani ilikuwa jibu kwa chapisho la Zlatan ambapo alimuanika mtu mwenye ushawishi ambaye alikuwa na shida naye mnamo 2018.


Muuzaji huyo alikuwa amejibu, “Huyu atampata anayemkokota na kumtengenezea mtindo. Hatutakuburuta ooo, beba kelele zako ingiza Aso Rock. Haithaminiwi hapa."


Alipoiona tweet hiyo, Zlatan alitafakari upya uamuzi wake huo na kwa ucheshi akashiriki tatizo lake mtandaoni, akiandika:


"Ninapotaka kutoa naangalia jinsi watu walivyotuma kunihusu hapo awali, jiunge. Huyu alinidhihaki 2020 na namuahidi 500k. Tunafanyaje kuwa hivi?”


 


 


 



RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved