logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Baada ya ukimya mrefu, Nyako aibuka kwenye TikTok Live kuomba msaada wa rent

"Mimi ninaomba mnisaidie tu kulipa rent, nimekuwa nje ya TikTok miezi mitatu hadi minne na ninarudi, zawadi bado ninahitaji kwa sababu nimeamua kujikimu kivyangu."

image
na MOSES SAGWEjournalist

Burudani19 March 2025 - 09:04

Muhtasari


  • Mara ya mwisho akifanya vipindi vya Live kwenye TikTok, Nyako alidokeza kwamba alikuwa anapambana na tatizo la moyo

Nyako Pilot

TIKTOKER Nyako aibuka tena kwenye mitandao huo baada ya ukimya wa takribani miezi minne, na safari hii ujio wake haujaja kwa kuchamba bali kwa unyenyekevu wa kuomba msaada.


Nyako ambaye alikuwa anajulikana kwa kutengeneza pesa nyingi kupitia vipindi vya mubashara kwenye mitandao huo wa video fupi alifanya video ya kutia huruma akiwalilia mashabiki wake kumsaidia na hela za kulipa kodi ya nyumba.


Nyako alisema kwamba kwa sasa angependa kujikimu kivyake na hataki hela za Wajerumani, akisema kwamba yuko tayari kupokea zawadi za TikTok ambazo baadae hugeuzwa kuwa hela.


"Mimi ninaomba mnisaidie tu kulipa rent, nimekuwa nje ya TikTok miezi mitatu hadi minne na ninarudi, zawadi bado ninahitaji kwa sababu nimeamua kujikimu kivyangu kimaisha mimi sitaki pesa za wajerumani nimeamua kujikimu kivyangu kimaisha," Nyako alisema.


Bila kueleza sababu ya kutoonekana kwenye TikTok kwa muda wa takribani siku 100, Nyako alisema kwamba sasa atarudi kwa kivumbi na kimbunga cha kipekee, lakini akasisitiza kwamba hawezi kata msaada wa zawadi kutoka kwa wafuasi wake.


"Hivyo mimi ninaomba hapo mahali tuliachia tuendelee hapohapo tunaendelea kwanza wakati huu ninarudi kwa njia ya kipekee kwa sababu vile mnajua tuko na jikoni kubwa, na nyumba ni kubwa hivyo tunarudi kwa ukubwa wa kipekee, hakuna matusi nimechoka kwenda kortini na watu na story ya kwenda kortini ilikua ikapiga kona ikaenda, sina muda wa hilo," alisema.


Mara ya mwisho akifanya vipindi vya Live kwenye TikTok, Nyako alidokeza kwamba alikuwa anapambana na tatizo la moyo, huku akiwatia wasiwasi mashabiki wake kwa kujitabiria kifo kwamba asingeishi muda mrefu.


Makala Zinazohusiana


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved