logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Michelle ni rafiki wangu wa karibu-Makena aweka mambo wazi

Aliongeza kuwa alikuwa chini ya shinikizo kubwa kutoka kwa jamii.

image
na Radio Jambo

Habari09 June 2021 - 11:04

Muhtasari


  • Mwandishi wa zamani wa BBC Makena Njeri amesema alikuwa akiishi uongo wakati alikuwa akichumbiana na wanaume
  • Makena alisema yuko sawa na watu wanaomwita "Chris au Christine"

Mwandishi wa zamani wa BBC Makena Njeri amesema alikuwa akiishi uongo wakati alikuwa akichumbiana na wanaume.

Makena ambaye hivi karibuni alijitambulisha kama 'shoga' alimwambia Massawe Japanni kuwa yuko sawa na uhusiano wake wa sasa.

"Sitaki kuzungumza juu ya suala hili kwani hiyo ni historia yangu na pia ilikuwa uhusiano wa kibinafsi sana."

Aliongeza kuwa alikuwa chini ya shinikizo kubwa kutoka kwa jamii.

"Shinikizo lilikuwa kubwa mno na nilikuwa naishi kwa uongo, na shida ni kwamba unaishia kumuumiza yule mtu mwingine."

Makena alisema yuko sawa na watu wanaomwita "Chris au Christine"

"Nina watu wanaoniita Chris na niko sawa na hilo."

Alipoulizwa juu ya kejeli kutoka kwa wanamitandao, Makena alisema;

"Niko sawa na maoni ya kila mtu. Inakuwa tu suala wakati inatumika kama silaha dhidi yako. ' Changamoto kubwa ni kwamba watu hawaelimishwi kuhusu jamii ya LQBTQ,"

Makena aliweka wazi kuwa Mitchelle sio mke wake, bali ni rafiki yake wa karibu.

"Ni makosa kubwa sana kumuita MItchelle mke wangu, uhusiano wangu na Mitchelle ni wa karibu sana, na sisi ni marafiki wa karibu

Ukiena kwenye mitandao yangu ya kijamii ya instagram nipakia picha za watu wengi,naishi maisha yangu kwa uwazi, kama kuna wakati utafika nimtambulishe mke wangu hadharani nitafanya hivyo." Alisema Makena.

 

 

 

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved