logo

NOW ON AIR

Listen in Live

'Hakuna mtu ambaye ni kamili,'Jemutai atoa sababu ya kumrudia na kumsamehe Hamo

Hii ni baada ya mmoja wa mashabiki wake kumuuliza kama alimsamehe Hamo.

image
na Radio Jambo

Makala23 July 2021 - 12:17

Muhtasari


  • Jemutai atoa sababu ya kumrudia na kumsamehe Hamo
  • Hii ni baada ya mmoja wa mashabiki wake kumuuliza kama alimsamehe Hamo
Jemutai & Hamo

Licha ya changamoto zilizokumba mapenzi yao miezi michache iliyopita wacheshi Profesa Hamo na Jemutai wameendelea kupiga hatua kubwakubwa katika juhudi za kuimarisha ndoa yao.

Wawili hao wamezidi kufichua mambo kadha wa kadha, huku kupitia kwenye mitandaoya kijamii ya youtube Je mutai akifichua sababu ya kumsamehe Hamo.

Hii ni baada ya mmoja wa mashabiki wake kumuuliza kama alimsamehe Hamo.

"Ndio nilimsamhe Hamo baada ya kugundua sisi sote tumekosa, na baada ya mazungumzo, hakuna mtu ambaye ni kamili ndio maana nilimrudia na hakuna mwanamke angependa kuona watoto wake wakiteseka,"

Pia mwingine aliuliza kwanini mchekeshaji Hamo amekuwa akimficha mke wake, na alikuwa na haya ya kusema;

"Mke wangu hapendi mambo ya mitandao ya kijamii sana, sijamficha, lakini kila kitu tunafanya miatndaoni huwa tunamwambia,"


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved