logo

NOW ON AIR

Listen in Live

'Mko na upuzi!' Karen Nyamu awashambulia mashabiki waliomkejeli kwa kuimba kibao cha Samidoh

Wanamitandao ya kijamii walimlaumu yeye na Samidoh kwa kumuumiza mke wa kwanza wa Samidoh.

image
na Radio Jambo

Makala06 August 2021 - 14:37

Muhtasari


  • Karen Nyamu awashambulia mashabiki waliomkejeli kwa kuimba kibao cha Samidoh

Mwanasiasa Karen Nyamu kupitia kwenye ukurasa wake wa instagram amewakashifu na kuwashambulia wanamitandao ambao wamekuwa wakimkejeli akiimba kibao cha baba wa mtoto wake Samidoh.

Mapema mwaka huu wawili hao waligonga vichwa vya habari baada ya kuthibitisha kwamba wana mtoto pamoja.

Wanamitandao ya kijamii walimlaumu yeye na Samidoh kwa kumuumiza mke wa kwanza wa Samidoh.

''Mko na upuzi. So, you people can sing to Samidoh's songs the way you want, but when I sing, it becomes violence?. [nyinyi mnaeza imba wimbo wa baba Sam vile mnataka , mimi nikiimba ni vayolence.] You are all mad. Yes you. Or you think he is a deadbeat, he disowned his son like most of your baby daddy?. I am not laughing at you but your brains are empty.'' Aliandika NYamu.

Ingawa mwimbaji huyo aliomba msamaha kwa mkewe wa kwanza, Karen ameshtumiwa kwa sababu ya kukataa kutoka kwake.

Wana mtoto pamoja na haijulikanikama wanasaidiana kumlea mtoto wao au la.

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved