'Kwani tunashare umaskini ama utajiri wa kujiwekelea,'Amira amuuliza mumewe Jimal

Muhtasari
  • Amira amshambulia mumewe baada ya kuchukua spika zake
Image: Studio

Mfanyabiashara Jimal na Amber Ray kwa mara nyingine wamegonga vichwa vya habari, baada ya madai ya kutengana kwao inaonekana kama Jimal alikuwa amempeza Amber Ray na ilibidi warudiane na mpenzi wake.

Aliandika ujumbe kwenye mitandao yake ya kijmaii akisema anapwza mtu huku kulingana na wanamitandao alikuwa anamaanisha Amber Ray.

Mkewe Jimal, Amira alipakia ujumbe akimuuliza mumewe nini haswa wanatumia na Amber Ray ni umaskini au ni utajiri wa kujiwekelea.

Hii ni baada ya maddai kwamba Jimal alichukua spika za mkewe na kumpelekea Amber Ray.

"Watu hawawezi pata kile wanachotaka,na niaje unaenda kupeana bidhaa za nyumbani, sasa mimi na Harman / kardo mpya! Sasa ikiwa ni spika Leo kesho sufuria pia? Kwani tunashare umaskini ama utajiri wa kujiwekelea Dunia ni ngumu smh'Amira aliandika," Amira alinakili.

Harman Kardon ni laini maarufu ya spika zinazoweza kugharimu Ksh 10,000 hadi zaidi ya Ksh 50,000.