logo

NOW ON AIR

Listen in Live

'Tayari najua mwanamume ambaye atanioa,'Saumu Mbuvi azungumzia kuolewa tena

Saumu yuko Dubai kwa harakati za kibiasara, akizungumzia hayo alisema kwamba  hana furaha

image
na Radio Jambo

Habari24 September 2021 - 14:52

Muhtasari


  • Saumu Mbuvi azungumzia kuolewa tena
  • Mapema mwaka huu Anwara na Saumu waliachana licha yao kubarikiwa na mtoto mmoja.

Saumu Mbuvi, alivuma mitanaoni baada ya kuachana na seneta Anwar, na kudai kwamba amekuwa akimdhulumu katika ndoa yake.

Kupitia kwenye ukurasa wake wa instagram, sekta ya Q&A alifichua kwamba anatazamia kuolewa, sio kuolewa tu bali alisema kwamba anamjua mwanamume ambaye atamuoa.

"Je unatazamia kuolewa tea," Shabiki aliuliza.

"Ndio pia najua yule atanioa tayari," Alijibu Saumu.

Saumu yuko Dubai kwa harakati za kibiasara, akizungumzia hayo alisema kwamba  hana furaha kwani ni mara yake ya kwanza kuwa mbali na watoto wake.

"Kwa sasa sina furaha,  i mara yangu ya kwanza kuwa mbali na watoto na familia yangu."

Mapema mwaka huu Anwara na Saumu waliachana licha yao kubarikiwa na mtoto mmoja.

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved