- Msanii B Classic ashambuliwa na mashabiki baada ya kudai anaacha muziki
Msanii kutoka kaunti ya Taita Taveta B Classic ni miongoni mwa wasanii chipukizi, ambao wamekuwa wakitia bidii katika kazi yao ya usanii kila kuchao.
B Classic ametoa vibao kadhaa ambavyo vimependwa na mashabiki mitandaoni.
Kupitia kwenye ukurasa wake wa instagram, msanii huyo amedai kwamba amewacha muziki kwani hajakuwa akishikwa mkono na mashabiki.
Msshabiki wengi hawajachukulia haya kama jambo la kushangaza bali asilimia kubwa wamedai kwamba ni kiki tu, kama vile wasanii wengine wamekuwa wakitafuta ili kutoa kibao kipya.
"Nimeacha muziki ๐ฐ Kwa sababu ya kuchanganyikiwa, hakuna msaada kutoka kwa mashabiki ๐ฐsijawahi fikiria kama ningechoka na kitu nakipenda hali ya Ila itawahimiza, kwa wale ambao waliamini poleni Labda siku moja mambo inaweza kubadilika. Bahati nzuri kwa hustle yangu mpya ๐ฐ๐ฐ๐ฐ," Aliandika B Classic.
KUlingana na video aliopakia kwenye ukurasa wake wa instagrama msanii huyo amedai kwamba amerudi kufanya kazi ya kutengeneza magari.
Mashabiki walikuwa na haya ya kusema;
baddi_money....: kiki za kifala sana๐๐๐
alex_karisa: mbona hupatikani kwa simu , usichoke mwana
seggyyusta: Ndima ni ndima, Bora kibala..
mwendwaamjukuu: Kiki๐๐๐
ondijo076: Hii ngoma inatoka lini๐ฅ
presenter_ali: Mwana Rudi bana tupige shughuli , usifanye hivyoo
mathew.alfred.1694: Naamn hiii bonge la song
lilmad._: ๐๐๐๐bro ambia watu ukweli...