logo

NOW ON AIR

Listen in Live

"Maisha yangu yalibadilika ulipowasili" Mulamwah aandikia bintiye ujumbe maalum huku akifichua sura yake hadharani kwa mara ya kwanza

Ameapa kupatia maslahi ya bintiye kipaumbele kila wakati huku akimtakia maisha marefu na  baraka tele maishani.

image
na Radio Jambo

Burudani25 October 2021 - 09:25

Muhtasari


•Mulamwah pamoja mpenzi wake Caroline Muthoni walipakia picha maridadi ya Keilah Oyando  kwenye kurasa zao za mitandao ya kijamii na kuambatanisha na jumbe maalum.

•Mulamwah ameapa kupatia maslahi ya bintiye kipaumbele kila wakati huku akimtakia maisha marefu na  baraka tele maishani.

Mchekeshaji David Oyando almaarufu kama Mulamwah hatimaye ametambulisha sura ya bintiye hadharani kwa mara ya kwanza tangu alipozaliwa takriban mwezi mmoja uliopita.

Mulamwah pamoja mpenzi wake Caroline Muthoni walipakia picha maridadi ya Keilah Oyando  kwenye kurasa zao za mitandao ya kijamii na kuambatanisha na jumbe maalum.

Msanii huyo mwenye umri wa miaka 28 alisema kwamba maisha yake yalibadilika punde baada ya binti yake kuzaliwa.

Ameapa kupatia maslahi ya bintiye kipaumbele kila wakati huku akimtakia maisha marefu na  baraka tele maishano.

"Malkia mwenyewe @keilah_oyando. Leo mniruhusu niringe na kifurushi changu cha furaha. Maneno hayawezi eleza jinsi alivyo mrembo. Maisha yangu yalibadilika punde ulipowasili. Maslahi yako yatakuwa ya kwanza kila wakati. Nakutakia maisha marefu na mafanikio. Asante @carrol_sonie kwa zawadi hii nzuri. Nawapenda nyote. Baraka." Mulamwah aliandika kwenye ukurasa wake wa Instagram.

Kwa upande wake Sonnie alionekana kupendezwa na urembo wa bintiye huku akimhakikishia kwamba mapenzi aliyo nayo kwake ni makubwa sana.

Wapenzi hao wawili walitangaza kuzaliwa kwa kifungua mimba wao kupitia mitandao ya kijamii mnamo Septemba 20.

"Na ni msichana. Muujiza umewasili.. maneno hayaweza kueleza ninavyohisi, ni kitu cha maana zaidi kuwahi fanyika maishani mwangu. Karibu kipenzi @keilah_oyando" Mulamwah aliandika kwenye ukurasa wake wa Instagram.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved