logo

NOW ON AIR

Listen in Live

'Nilidanganya nilikuwa mjamzito,ataachwa tu,'Shakilla amshambulia Miss P

Kulingana na Shakilla, pia naye alidanganya kuwa na ujauzito awali ilhali hakuwa na ujauzito wowote.

image
na Radio Jambo

Habari01 November 2021 - 21:06

Muhtasari


  • Kulingana na Shakilla, pia naye alidanganya kuwa na ujauzito awali ilhali hakuwa na ujauzito wowote

Mwanasholaiti chipukizi Shakilla, kupitia kwenye mitandao yake ya kijamii ya instagram, amefutilia mbali madai kwamba Eric Omondi amempachika msanii Miss P ujauzito.

Kulingana na Shakilla, pia naye alidanganya kuwa na ujauzito awali ilhali hakuwa na ujauzito wowote.

Huku baada ya kufunguka aliendelea kumkejeli Miss P, kwa kutokuwa makini, kuwadanganya mashabiki.

Shakilla alimwambia Miss P wakati mwingine aweze kumuajiri mhariri mzuri ambaye anajua kazi vyema, kwani ujauzito wake haukuwa umechorwa vizuri.

"Kwanza ilikuwa ni mimi ambaye nilidanganya kwamba nina ujauzito wa malkia wao,baada ya kufanya hayo mara nyingi ili video iwe njema alafu naona picha ya msichana ambayo haijaharriwa vyema akisema amechukuliwa

Wakati mwingine ni afadhali ununue kivimbe cha mtoto,ama upate mhariri mzuri, kuwajibika kitu gani, mwambie atatumiwa na kisha aachwe baada ya video uoata watazamaji wengi," Alisema Shakilla.

Katika chapisho nyingine Shakilla alimkejelli Eric Omondi, kwa kusema kwamba atawajibika, huku akishindwa kwani hakuogopa kufunga goli mahali kila mtu alikuwa anafunga.

"Hauogopi kufunga mahali mwanamume mwingine alifunga kupia free kick, na kila goli ambazo ziko ili sisi tujue kwamba huwa anaimba

Niliimba 'sunday school' na hamna mtu yeyote alikuwa hapo wa kunisaidia, lakini kwa nini najisumbua hawezi fikia wasanii wa kenya."

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved