logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Wanawake wengi wananiomba niwapachike ujauzito- Mulamwah adai

Hata hivyo ameamua kuvunja nyoyo za wanadada hao kwani ametangaza hana nia ya kutimiza maombi yao.

image
na Radio Jambo

Habari10 November 2021 - 08:48

Muhtasari


•Mchekeshaji huyo ambaye pia ni muuguzi amedai kwamba amekuwa akipokea jumbe nyingi kutoka kwa wanadada wanaomezea mate kupachikwa ujauzito naye.

•Hata hivyo ameamua kuvunja nyoyo za wanadada hao kwani ametangaza hana nia ya kutimiza maombi yao

David Oyando almaarufu kama Mulamwah

Takriban mwezi mmoja unusu baada ya Mulamwah kukaribisha kifungua mimba wake duniani, mchekeshaji huyo sasa ametoa madai kuwa wanatamani kupata mtoto pamoja naye.

Kupitia kurasa zake za mitandao ya kijamii, mchekeshaji huyo ambaye pia ni muuguzi amedai kwamba amekuwa akipokea jumbe nyingi kutoka kwa wanadada wanaomezea mate kupachikwa ujauzito naye.

"Wanadada wengi wananitumia jumbe wakitaka kupata watoto nami" Mulamwah amedai.

Hata hivyo ameamua kuvunja nyoyo za wanadada hao kwani ametangaza hana nia ya kuwatimizia maombi yao.

Ujumbe huo wa baba huyo wa mtoto mmoja umeibua gumzo kubwa mitandaoni wengi wakionekana kuwa na ushauri wa kumpatia msanii huyo.

@Mwendiajnr Wanataka pesa zako kaka

@Githui_254 Tafadhali watume kwa DM yangu, pia mimi sina masikio

@ukonangapi Unaringa kuhusunini jamaa

@fanuel_ Kutafuta kiki ni ugonjwa!

Mulamwah pamoja na mpenzi wake Carrol Sonnie walibarikiwa na mtoto wa kike, Keilah Oyando mnamo Septemba 20.

"Na ni msichana. Muujiza umewasili.. maneno hayaweza kueleza ninavyohisi, ni kitu cha maana zaidi kuwahi fanyika maishani mwangu. Karibu kipenzi @keilah_oyando" Mulamwah aliandika kwenye ukurasa wake wa Instagram mtoto alipozaliwa.

Mchekeshaji huyo alieleza raha kubwa  ambayo alipata moyoni baada ya kubarikiwa na mtoto wake wa kwanza  huku akidai kuwa siku itimiapo ataonyesha urembo wa bintiye hadharani.

"Ni mrembo, siwezi subiri kuonyesha walimwengu siku moja na niwe na mazungumzo ya baba na binti. Mimi ni baba mwenye raha. Shukran kwa Mungu" Alisema Mulamwah.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved