- Kulingana na KRG, alijaribu kadiri alivyoweza kuokoa ndoa hiyo lakini yote yalikuwa bure
- Alisema kuwa Lina hangebadilika na hakuna njia ambayo wanaweza kutengeneza familia nzuri.
- Inavyoonekana, wawili hao bado 'wanapigana' na wanatumia kurasa zao za Instagram kutukanana
Mapema mwezi uliopita, msanii chipukizi KRG the Don alifichua kwambaanampa mkewe talaka rasmi kwa sababu tu amekuwa akijihusisha na vitendo vya uasherati nyuma yake.
Kulingana na KRG, alijaribu kadiri alivyoweza kuokoa ndoa hiyo lakini yote yalikuwa bure.
Alisema kuwa Lina hangebadilika na hakuna njia ambayo wanaweza kutengeneza familia nzuri.
Inavyoonekana, wawili hao bado 'wanapigana' na wanatumia kurasa zao za Instagram kutukanana.
Siku chache zilizopita, Lina aliacha post nyeti kwenye Instagram akisema kuwa 'mtu anataka umlelee watoto na kumbe hajui nguvu za kiume'.
Kwa kweli, ujumbe huo ulikuwa ukielekezwa moja kwa moja kwa KRG na leo, aliamua kujibu.
KRG alishinda kwa nini mkewe anazidi kukonda, huku akiuliza kama atakua hai mwishoni mwa mwaka huu.
"kwa nini watu wanakonda hivi? na mwezi haijaisha, chakula ndio shida au ni kumeza ndio shida,je?baada ya mwaka tutakua bado tupo au watu watakuwa wamejitia vitanzi,"Aliandika KRG.
Pia msanii huyo alishindwa kwa nini watu wanakasirika baada ya kuuliza swali hilo au kumkejeli mkewe, ilhali rafiki zake ndio wanamkejeli zaidi.
"Kwa nini watu wanakasirika?nilikuwa nasema kwa maana marafiki zake ndio walinitumia picha,za shosh ati anakula ngumu na kuvalia viatu vikubwa sana
Mara amekonda na mashavu yamekusha, kwa hivyo niliamua kuandika hapa ili atie bidii ya kumeza chakula wawache kuona hizo vitu negative."