Kieleweke Jimal sio mume wangu-Amira apasua mbarika

Muhtasari
  • Mfanyabiashara huyo amewataka watu kuacha kumhusisha na Jamal kwani yeye sio mume wake
Image: INSTAGRAM

Mwenyekiti wa Chama cha Matatu cha Nairobi Jamal Ibrahim maarufu kama Jimal Roho Safi amenaswa kwenye video pamoja na aliyekuwa mpenzi wake Amberay.

Video hiyo imewafanya wengi kumwita Amira, ambaye amejibu kwa kudai kuwa yeye na Jimal hawako pamoja tena.

 Mfanyabiashara huyo amewataka watu kuacha kumhusisha na Jamal kwani yeye sio mume wake tena na anachofanya si kazi yake tena.

"Ninashughulikia hili kwa mara ya mwisho kabisa!! acha kunihusisha na Jamal. Unahitaji kuacha kuniburuza kwa kila suala ambalo unaona huko nje, sisi hatuyuko pamoja,

Mimi sio mke wake, yeye sio mume wangu,  mimi sio shida yake, yeye sio shida yangu tena. Ninawajibika tu na kuwajibika kwa watoto wangu!! KIELEWEKE!!" Amira Alisema.

Watatu hao waligongwa vichwa vya habari mara tu baada ya Jimal Kumuoa mwanasoshaolaiti Amber Ray, huku wakizidi kuwa gumzo ya mjini baada ya kuachana tena.