'Nikejeli na jambo jipya,'Rue Baby amshambulia shabiki aliyekejeli mwili wake

Muhtasari
  • Rue Baby amshambulia shabiki aliyekejeli mwili wake
  • Watu wengine ni chuki tu na wataendelea kukupa nguvu hasi kwa kutuma maoni hasi
  • Hata hivyo hakuna aliyekamilika na watu wanapaswa kujifunza kuthaminiana
64781306_134343814430837_5882671972455945431_n
64781306_134343814430837_5882671972455945431_n

Kukejeli na Kutia aibu mwili  wa msanii kumekuwa jambo la kawaida katika kurasa za mitandao ya kijamii. Sio kila mtu anafurahi kukejeliwa na mashabiki mitandaoni.

Watu wengine ni chuki tu na wataendelea kukupa nguvu hasi kwa kutuma maoni hasi.

Hata hivyo hakuna aliyekamilika na watu wanapaswa kujifunza kuthaminiana.

Binti ya Akothee Rue pia hajaachwa. Rue ni mmoja wa wanamitindo bora nchini Kenya.

Rue pia ni mshawishi mkuu wa chapa. Leo hii Rue akiwaanatangaza  kazi yake kama mshawishi wa chapa ya Bikini, shabiki mmoja hangeweza kusaidia na aliamua kutoa maoni hasi kuhusu chapisho la Rue.

Shabiki huyo alimwambia Rue kuwa kifua chake kipo tambarare na hana matiti.

Rue aliangazia Maoni ya Mashabiki kwenye ukurasa wa hadithi za Instagram na amefichua kuwa anapenda sana kuzuia maoni hasi maishani mwake.

Rue aliweka tena picha yake akiwa ndani ya Bikini na kuwataka mashabiki kushambulia kwa kitu ambacho hawakifahamu kwa sababu anafahamu kuwahana kitambi.

"Nawapa block nyinyi nyote wajinga ambao mmekuja kwenye ukurasa wangu na kuongea vitu ni kama hamana akili, sina matiti, ni kitu ambacho kiko nje, na kila mtu anajua

Nina ifua tambarare na ni kitu nyinyi nyote mnajua, ni kejeli na kitu kipya," Alisema Rue.