logo

NOW ON AIR

Listen in Live

"Wakae chini waelewane" Mzee Abdul amsihi mwanawe Diamond Platnumz amalize ugomvi wake na Harmonize

Mzee Abdul alisema hana kinyongo chochote dhidi ya mwanawe wala mpenzi wake wa zamani, Mama Dangote kwani alishawasamehe na kusahau yaliyopita.

image
na Radio Jambo

Dakia-udaku29 November 2021 - 09:44

Muhtasari


•Mzee  Abdul alimsihi Diamond ashiriki kikao na Harmonize wazungumzie tofauti zao na waelewane.

•Mzee Abdul alisema hana kinyongo chochote dhidi ya mwanawe wala mpenzi wake wa zamani, Mama Dangote kwani alishawasamehe na kusahau yaliyopita.

Diamond Platnumz, Mzee Abdul, Harmonize

Baba mzazi ya Diamond Platnumz, Mzee Abdul Juma  ametoa wito kwa mwanawe kuelewana na mwenzake wa zamani Rajab Abdul Kahali almaarufu kama Harmonize.

Alipokuwa kwenye mahojiano na Mbengo TV hivi majuzi, mzee  Abdul alimsihi Diamond ashiriki kikao na Harmonize wazungumzie tofauti zao na waelewane.

Mzee huyo ambaye alitengana na mamake Diamond, Mama Dangote miaka mingi iliyopita ameomba serikali na walio karibu na nyota wale wawili wa Bongo kuwapatanisha kuona kuwa wote wanaipeperusha bendera ya Tanzania.

"Wakae tu waelewane, hii dunia ni mapito basi. Yakitokea maneno kama haya wanaotoa hisia wawaagize waelewane wawe pamoja. Alafu tena waziri wa michezo kama yupo vilevile kuna uwezekano wa kuwaita. Mama Naseeb Sanura na Shamte kama wana uwezo wanaweza wakawaita wakaomgea, wakawaweka chini. Watoto  kama watawasikiliza waongee kama ndugu waelewane"  Alisema Mzee Abdul.

Mzee Abdul alisema hana kinyongo chochote dhidi ya mwanawe wala mpenzi wake wa zamani, Mama Dangote kwani alishawasamehe na kusahau yaliyopita.

Siku kadhaa zilizopita Harmonize alifunguka kuhusu ugomvi wake na aliyekuwa bosi wake katika WCB Diamond Platnumz.

Konde Boy alisema Diamond pamoja na mameneja wake walianza kumuonea gere wakati nyota yake ilianza kung'aa zaidi hadi akatangaza vita dhidi yake.

"Aliniambia eti 'mimi nikimpa mtu heshima yangu, asiponirudishia naichukua kinguvu. Unataka kushindana na mimi na huniwezi kiserikali, huniwezi kihela na huniwezi kiuchawi. Nipe mkono tushindane.' Mimi nilibaki nimeduwa nikajiuliza kama tumefikia hatua hiyo keshoye mtu angeweza kuniwekea sumu nikafa" Alisema Harmonize

Harmonize alisema kabla yake kutoka Wasafi alikuwa amejaribu sana kurejesha uhusiano mzuri na Diamond bila mafanikio.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved