logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Size 8 aunga mkono muswada wa Eric Omondi unaopendekeza kukuzwa kwa muziki wa Kenya

Amesema ukuzaji wa sekta ya muziki hapa nchini utakuwa wa msaada mkubwa haswa kwa kizazi kipya ikiwemo watoto wake iwapo wataamua kujitosa katika muziki.

image
na Radio Jambo

Yanayojiri06 December 2021 - 07:04

Muhtasari


•Amesema ukuzaji wa sekta ya muziki hapa nchini utakuwa wa msaada mkubwa haswa kwa kizazi kipya ikiwemo watoto wake iwapo wataamua kujitosa katika muziki.

Mwanamuziki wa nyimbo za injili Linet Munyali almaarufu kama Size 8 ameunga mkono muswada unaosukumwa na Eric Omondi ambao unapendekeza vituo na maeneo ya burudani nchini kucheza 75% ya muziki wa hapa Kenya.

Alipokuwa anazungumza na wanahabari siku ya Jumapili, Size 8 alisema angependa muswada huo upitishwe kwani vituo vya burudani hapa nchini hupendelea sana kucheza muziki wa kimataifa.

Mke huyo wa mcheza santuri DJ Moh amesema ukuzaji wa sekta ya muziki hapa nchini utakuwa wa msaada mkubwa haswa kwa kizazi kipya ikiwemo watoto wake iwapo wataamua kujitosa katika muziki.

"Hatuwezi kataa hiyo kwa sababu Kenya ni mojawapo wa nchi chache ambapo muziki unaochezwa kwa redio sanasana si wa hapa nchini. Ukienda Uganda, 90% ya muziki unaochezwa ni wa pale, ukienda Afrika Kusini, Nigeria na Tanzania wanacheza  90% ya muziki wa pale. Hatuungi muswada huu mkono kwa ajili yetu binafsi, hata watoto wetu kina Ladasha wakitaka kuimba atasaidika. Acha tukuze muziki kwa sababu kuna wasanii wengi chipukizi" Alisema Size 8.

Mwanamuziki huyo alishawishi vyombo vya habari kucheza muziki wa Kenya zaidi huku akisema angependekeza vicheze asilimia 90%.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved