logo

NOW ON AIR

Listen in Live

"Hatujazungumza miaka miwili!" Mkewe Mr Seed afunguka kuhusu uhusiano wake na Diana Marua

Alisema alikosa kuhudhuria hafla ya kuzindua Diana kama mwanamuziki kwa kuwa mwaliko ulikuja kuchelewa na tayari alikuwa na mipango mingine.

image
na Radio Jambo

Yanayojiri07 December 2021 - 07:30

Muhtasari


•Nimo  alifichua hakujakuwa na mawasiliano yoyote kati yake na Diana kwa kipindi cha takriban miaka miwili iliyopita wala kukutana ana kwa ana.

•Alisema alikosa kuhudhuria hafla ya kuzindua Diana kama mwanamuziki kwa kuwa mwaliko ulikuja kuchelewa na tayari alikuwa na mipango mingine.

Diana Marua na Nimo Gachuiri

Bi Nimo Gachuiri ambaye ni mke wa mwanamuziki  mashuhuri Mr Seed hatimaye amemwaya mtama kuhusu uhusiano wake wa sasa  na mke wa Bahati Diana Marua. 

Alipokuwa kwenye mahojiano na Nicholas Kioko, Nimo aliweka wazi kwamba hana ugomvi wowote na rapa huyo chipukizi. 

Nimo  hata hivyo alifichua hakujakuwa na mawasiliano yoyote kati yake na Diana kwa kipindi cha takriban miaka miwili iliyopita wala kukutana ana kwa ana.

"Kusema kweli hatujazungumza na Diana kwa kipindi cha miaka miwili sasa. Hatujawahi kuongea, hatujawahi kutana ana kwa ana. Mimi sina ugomvi na yeye. Nahisi hakuna haja ya kuzozania mambo yaliyotendeka miaka miwili iliyopita. Ni ufala." Nimo alisema.

Mama huyo wa mtoto mmoja alisema ingawa hajawahi kupiga hatua ya kumfikia Diana ili wasuluhishe mzozo wao, tayari amekubali kusahau yaliyopita.

Alisema alikosa kuhudhuria hafla ya kuzindua Diana kama mwanamuziki kwa kuwa mwaliko ulikuja kuchelewa na tayari alikuwa na mipango mingine. Hata hivyo alisema alifuatia hafla hiyo.

"Nilikuwa nimealikwa. Baha alianiambia Jumapili. Nilikuwa na mipango mingine  siku hiyo. Nilikuwa nahudhuria hafla ya kanisa. Kulikuwa na dress code na unajua sisi wanawake hatuwezi kutokea hivo tu. Nilifuatilia lakini nyuma ya pazia" Nimo alisema.

Nimo alisema hatua ya Diana kujitosa kwenye muziki ni nzuri huku akimhimiza asikufe moyo kutokana na chuki dhidiyake mitandaoni.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved