logo

NOW ON AIR

Listen in Live

'2022 Wanaume tupunguze mshene,'Arrow Bwoy asema baada ya habari za Nadia kuwa mjamzito kufichuliwa

Habari hizo zimepokelewa na hisia tofauti miandaoni huku baadhi ya mashabiki wakiwapongeza wawili hao

image
na Radio Jambo

Yanayojiri05 January 2022 - 11:56

Muhtasari


  • Arrow Bwoy asema haya baada ya habari za Nadia kuwa mjamzito kuenea
  • Habari hizo zimepokelewa na hisia tofauti miandaoni huku baadhi ya mashabiki wakiwapongeza wawili hao

Msanii Arrow Bwoy ameoneana kugadhabishwa na habari zilizofichuliwa na mcheshi Jalang'o kuwa mpenzi wake Nadia ana ujauzito wake.

Katika kipindi chake cha asubuhi  kwenye Kiss FM, Jalang’o alimtaka Mukami kukoma kuficha madai ya ujauzito wake kwa kuvaa masweta ya kubebea akiongeza kuwa ujauzito huo ungeonekana hivi karibuni.

“Nadia pia sasa itabidi awache kuvaa masweater…wacha mimba tu itoke tu…mimba ni kama kohozi hauwezi zuia, ikibidi ukohoe utakohoa tu..”

Arrow Bwoy alijibu habari hiyo kwa maneno makali.

"2022 wanaume tupunguze mshene bana biashara haikuhusu achana nayo kabisa shugulika na maisha yako," Msanii huyo alisema.

Habari hizo zimepokelewa na hisia tofauti miandaoni huku baadhi ya mashabiki wakiwapongeza wawili hao.

Siku chache zilizopita, mmoja wa mashabiki wa Nadia alimuuliza ujauzito wake uko wwapi baada ya kupakia picha mitandaoni ambapo Nadia alimjibu na kusema kuwa;

"hebu tuulize Ronaldo ni kama tumeiacha kwa field kesho siataisahau nitakuletea unibebee nisiisahau tena.”

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved