- Chris Kirwa amshauri Holy Dave kuoa kabla siku ya Valentine
Mratibu wa hafla Chris Kirwa Jumanne alimshauri mwimbaji wa Injili Holy Dave kuhakikisha ameoa kabla siku ya wapendao 'Valentine'
Kupitia ukurusa wa Instagram wa Holy Dave, kwenye sehemu ya maoni, Chris kirwa alinakili kwamba atafute mke ili ifikiapo siku ya wapendanao awe angalau na mtu wakushauriana naye.
" Indomie iwezi kusaidia,Tafuta mtu nani, baridi ya Valentine inakaribia." Kirwa aliandika kwenye sehemu ya maoni ya Holy Dave
Kufuatia kauli hiyo, Holy Dave alijitokeza na kujibu kwa ucheshi kwamba Chris kirwa ameamua kumtoanisha mwaka huu mpya, huku akiwa pongeza Gardian Angel kwa kufunga ndoa na mpenzi wake wa siku nyingi Esther Musila.
Aidha, aliwambia mashabiki wake pia yeye ako njiani kupata mchumba.
"Hizi vita mnaanza nazo 2022 staki. HD hapangwingi. lakini mbona uongo. Valentine hainipati hivi... Hongera kwa Esther Musila na Gardian Angel, Mimi ndiye nafuata sasa" Holy Dave alisema kupitia ukurusa wa instragram
Holy Dave anafahamika sana mitandaoni kutokana na upishi wake, ambao amekuwa akipakia kwenye ukurasa wake wa instagram kwa muda sasa.
Pia ni miongoni mwa watu mashuhuri ambao maisha yao ya mapenzi hayajakuwa mitandaoni.