logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Lupita Nyong'o apatikana na Virusi vya Korona

kupitia ukurasa wake wa twitter, Jumanne alipimwa na kupatikana na virusi hivyo vya Korona licha ya kupata chanjo.

image
na

Yanayojiri05 January 2022 - 07:11

Muhtasari


•Lupita apimwa na kupatikana na virusi hivyo vya Korona licha ya kupata chanjo kikamilifu.

lupita-nyongo1

Muigizaji wa Hollywood na Mshindi watuzo ya Oscar,Lupita Nyongo amepimwa na kukutwa na virusi vya uviko-19 

Lupita, kupitia ukurasa wake wa twitter, Jumanne alipimwa na kupatikana na virusi hivyo vya Korona licha ya kupata chanjo.

 Katika tangazo hilo alisema kwa sasa  amejitenga na watu kuzuia kueneza virusi hivyo na akasema anatarajia kupata nafuu hivi karibuni.

" Mimi pia nimethibitishwa kuwa na Covid-19. nimechanjwa kikamilifu. nimejitenga na ninaamini nitakuwa mzima."

 

 Lupita aliwaomba mashabiki wake watahadhari  na virusi hivi vya Korona "Tafadhali fanya yote uwezayo ili kujilinda wewe na wengine dhidi ya magonjwa hatari."

 Kutokana na virusi hivyo, Hollywood imelazimika kuhairisha majojiano ya matangazo ya filamu mpya  'The 355' ilikuzingatia kupona kwa nyota wao

Lupita ni miongoni mwa waigizaji waliotarajiwa katika Tamasha la kusisimuliwa  lililotarajiwa kufanyika Ijumaa. Wengine waliokuwa kuwa kwenye orodha hio ni ikiwemo na   Jessica Chastain, Penelope Cruz, Diane Kruger, na Bingbing Fan.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved