logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Mapenzi yashinda! Guardian Angel na mpenziwe Esther Musila wafunga pingu za maisha

Bi Musila alisherehekea hatua waliyopiga na mpenzi wake huku akimtaja mwanamuziki huyo mwenye umri wa miaka 31 kama mtu maalum na rafiki wake wa dhati.

image
na Radio Jambo

Habari04 January 2022 - 19:37

Muhtasari


•Wawili hao walifanya harusi ya faragha iliyohudhuriwa na wanafamilia na marafiki wachache mnamo Jumanne  tarehe 4  mwezi Januari, 2022

•Bi Musila alisherehekea hatua waliyopiga na mpenzi wake huku akimtaja mwanamuziki huyo mwenye umri wa miaka 31 kama mtu maalum na rafiki wake wa dhati.

Guardian Angel, Esther Musila

Hatimaye mwanamuziki wa nyimbo za injili Peter Omwaka almaarufu kama Guardian Angel na mpenzi wake Esther Musila  wamefunga ndoa rasmi.

Wawili hao walifanya harusi ya faragha iliyohudhuriwa na wanafamilia na marafiki wachache mnamo Jumanne  tarehe 4  mwezi Januari, 2022

Guardian Angel na Bi Musila walitumia kurasa zao za mitandao ya kijamii kufahamisha walimwengu kuhusu hatua hiyo muhimu ambayo walipiga.

"Na katika siku ya kuadhimisha kuzaliwa kwangu, Mungu alinitendea tena. Bw na Bi Omwaka... mke wangu @esther.musila" Guardian Angel alitangaza kupitia ukurasa wake wa Instagram.

Bi Musila alisherehekea hatua waliyopiga na mpenzi wake huku akimtaja mwanamuziki huyo mwenye umri wa miaka 31 kama mtu maalum na rafiki wake wa dhati.

Kwenye chapisho lake Instagram, Malkia huyo mwenye umri wa miaka 51 alikiri kamwe maishani hakuwahi kufikiria kwamba angepatana na mpenzi kama Guardian Angel.

"Kupata mtu maalum kama wewe kati ya watu wote ulimwenguni ni jambo ambalo sikuwahi kufikiria. Wacha tufanye maisha haya pamoja. Bw na Bi Omwaka" Esther aliandika.

Wanandoa hao wawili wamekuwa katika mahusiano kwa kipindi cha takriban miaka miwili na  wamekuwa wakijivunia maamuzi waliyofanya ya kuwa pamoja licha ya ukosoaji mkubwa ambao wamekabiliana nao  kufuatia pengo kubwa kati ya umri wao.

Esther ana watoto wawili wakubwa kutoka kwa ndoa yake ya hapo awali. Aliyekuwa mume wake na ambaye ni baba ya watoto wake watatu aliaga dunia takriban miaka mitano iliyopita.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved