logo

NOW ON AIR

Listen in Live

(+Picha) Jinsi ilivyokuwa katika harusi ya Guardian Angel na Esther Musila

Guardian Angel kwa wakati huo alionekana kuwezwa na hisia na kutirirkwa na machozi ya furaha

image
na Radio Jambo

Habari05 January 2022 - 09:56

Muhtasari


•Guardian Angel kwa wakati huo alionekana kuwezwa na hisia na kutiririkwa na machozi ya furaha

Guardian Angel amvisha pete Esther Musila

Hatimaye Guardian Angel na Esther Musila walifunga pingu za maisha siku ya Jumanne katika hafla ya faragha iliyofanyika katika uwanja wa Sue Gardens eneo la Muthaiga.

Wapenzi hao wawili ambao wamekuwa wakichumbiana kwa kipindi cha takriban miaka miwili walivishana pete mbele ya wanafamilia na marafiki wachache .

Katika video iliyochapishwa Instagram na mmoja wa marafiki zao, mwanamuziki Timeless Noel, Bi Musila alionekana akionekana akiongozwa na mwanawe mkubwa  hadi kwa mume wake Guardian Angel .

Musila alitembea kwa mwendo wa aste aste hadi pahali mpenzi wake alikuwa amemsubiri huku muziki aina ya Jazz ukicheza.

Guardian Angel kwa wakati huo alionekana kuwezwa na hisia na kutirirkwa na machozi ya furaha. Mwanamume aliyekuwa amemsimamia alionekana akimsaidia na kitambaa cha kufutia machozi.

Ilikuwa siku maalum kweli kwa familia ya Omwaka kwani pia walisherehekea siku yake ya kuzaliwa anapohitimu miaka 33.

Wanamitandao wameendelea kuwasherehekea wapenzi hayo kwa hatua kubwa ya maisha ambayo walipiga.

@blessednjugush Kheri njema, Hongera

@timelessnoel najivunia kuwa emcee.. Hongera ndugu

@kambuamuziki Anayepata mke

@magreatmumbi Mapenzi tight kama kifuniko ya gas.. walisema mtaachana lakini watangoja sana.. eeh

@dkkwenyebeat Hongera

@mojishortnbabaa Hongera


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved