logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Huddah Monroe awapa onyo kali marafiki ambao hawaungi mkono biashara yake

Kutokana na tabia hio ya omba omba  mrembo huyo amewaonya kwamba wasisikie vibaya endapo akakatiza mazungumzo nao.

image
na

Yanayojiri06 January 2022 - 06:07

Mwanasoshalaiti na mfanyibiashara maarufu humu nchini Alhuda Njoroge almaarufu Huddah Monroe  amefunguka wazi na kusema ni jambo la kushangaza kuona marafiki wengi aghalabu ndio huwa wanakosa kununua bidhaa ambazo mtu anauza.

Kupitia ukurusa wake wa Instagram, Huddah ameeleza kero kwamba wanaojiita watu wa familia na wale marafiki zake hawapendi kumsaidia kwa kuendeleza biashara yake 

"Kitu cha kuchekesha ni kwamba watu wanaonunua bidhaa zangu sio marafiki au familia yangu. Marafiki wawili au watatu ndio tu hufanya hivyo " Alisema

Alisema wanaomuunga mkono kwa kiwango kikubwa ni watu ambao hawajuani na ambao si marafiki zake huku akieleza kazi ya marafiki nikumuomba vitu bila malipo.

"Ni wageni wanaoniunga mkono. Marafiki zangu daima huomba vitu vya bure na huwa hawataki niseme" Alisema Huddah

Kutokana na tabia hio ya omba omba  mrembo huyo amewaonya kwamba wasisikie vibaya endapo akakatiza mazungumzo nao.

"Ikiwa haununui bidhaa zangu, ninakukata" Huddah aliwambia marafiki zake

mrembo huyo tajiri ambaye amekuwa Dubai karibu miaka miwili, alisema kwamba msaada wake mwingi hutoka kwa watu wasiowajua na sio marafiki na familia yake. ,” Huddah alichapisha.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved