logo

NOW ON AIR

Listen in Live

"Zaa wako unyoe!" Vera Sidika aapa kutopitisha wembe kichwani mwa bintiye kamwe

Vera ambaye anajulikana kutowapa nafasi wakosoaji amewaarifu wale ambao hawaridhishwi na jinsi anavyotunza nywele ya bintiye  ya 'Kiarabu' wamkome na waangazie watoto wao wenyewe.

image
na Radio Jambo

Habari06 January 2022 - 08:13

Muhtasari


•Vera ambaye anajulikana kutowapa nafasi wakosoaji amewaarifu wale ambao hawaridhishwi na jinsi anavyotunza nywele ya bintiye wamkome na waangazie watoto wao wenyewe.

•Amewaomba wale  wanaomwambia aache kujigamba na nywele ya kwanza ya bintiye wamkome kwani hana mpango wowote wa kubadilisha mawazo yake wakati wowote kutoka sasa.

Mwanasoshalaiti Vera Sidika amewajibu baadhi ya wanamitandao ambao wamekuwa wakimshinikiza anyoe kichwa cha binti yake Asia Brown,

Kupitia mtandao wa Instagram, kikundi kikubwa cha wanamitandao kimekuwa kikimkosoa mama huyo wa mtoto mmoja kwa kuachilia nywele ambayo binti yake alizaliwa nayo iendelee kumea huku wengine wakimweleza itabadilika pindi tu atakapomnyoa.

Vera ambaye anajulikana kutowapa nafasi wakosoaji amewaarifu wale ambao hawaridhishwi na jinsi anavyotunza nywele ya bintiye  ya 'Kiarabu' wamkome na waangazie watoto wao wenyewe.

"Zaa wako unyoeee!! Kama uko naye basi muangalie yeye. Usiniambie jinsi nitalea mtoto wangu!" Vera aliwajibu wanamitandao waliomwomba anyoe bintiye.

Mwanasoshalaiti huyo mwenye umri wa miaka 32 ameapa kwamba kamwe hatawahi kukaa nywele ya binti yake.

Amewaomba wale  wanaomwambia aache kujigamba na nywele ya kwanza ya mtoto huyo mwenye umri wa miezi miwili kwa sasa wamkome kwani hana mpango wowote wa kubadilisha mawazo yake wakati wowote kutoka sasa.

"Afadhali mkome kuniambia  'ngoja hadi unyoe nywele kwanza na uone jinsi itakavyoonekana' Hapana. Sitamkata nywele kamwe. Hilo nimeamua!! Nyinyi nyote endelea na kukata nywele za watoto wako. Nikose hapo" Vera alisema.

Mwanasoshalaiti huyo alifichua sura ya bintiye kwa mara ya kwanza mnamo Desemba 20 na amekuwa akionyesha ulimwengu wote urembo wake kila uchao tangu siku hiyo.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved