•Dada yangu kajala ..Amenisumbua sana kwa muda wa karibia mwaka mzima ananiuliza kaka unafanyaje kupungua nikawa namwambia siri ni mazoezi na lishe bora
•Amefurahi sana kukutana na mimi na amefurahia mazoezi niliyompa. nina imani atapungua sasa na kufikia mwili wa ndoto yake
Mwanamuziki wa Bongo Peter Msechu siku za hivi karibuni ameonekana na mwanamtindo Kajala Masanja huku akidai mazoezi aliyompa Kajala ameyapenda.
Kupitia ukurusa wake wa Instagram, Msechu amewajibu mashabiki ambao wamekuwa wakitaka kujua kinachoendelea baina yake na Kajara.
Kulingana naye alisema Kajara amekuwa akitaka kujua siri ya kupunguza ukubwa, na hivyo akamuomba aweze kumsaidia kupunguza uzani wake
"Dada yangu kajala ..Amenisumbua sana kwa muda wa karibu mwaka mzima ananiuliza kaka unafanyaje kupungua nikawa namwambia siri ni mazoezi na lishe bora akaniambia naomba unisaidie na mimi kwenye mazoezi nipungue nikawa busy sana sana sikupata muda kabisa." alisema Msechu
Vile vile. alidokeza kilichomfanya ajitolee mwaka huu kumpeleka Kajala kumfundisha mazoezi.
"Akawa ananipigia simu analia sana hadi makamasi yanamshuka anasema kaka unanionea, yaani kunipa dakika kadhaa tu unifundishe mazoezi yako, unashindwa. nikawa namwambia Kajala tulia usilie jamani futa makamasi akawa ananyamaza basi mwaka huu ndio nikasema nimuonee huruma walau leo nimpe mazoezi hapa @adreline255 kidogo."
Isitoshe alieleza baada ya kumpeleka kwenye mafunzo hayo, Kajara akuweza kuficha furaha aliyokuwa nayo huku akimwahidi atapungua na kufikia mwili wa ndoto yake
"hivyo leo amefurahi sana kukutana na mimi na amefurahia mazoezi niliyompa. nina imani atapungua sasa na kufikia mwili wa ndoto yake"