logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Konde Gang ya Harmonize yamwachilia Country Boy

Msimamizi wa lebo ya Konde Gang msanii Harmonize ametangaza kusitisha uhusiano wa kazi na msanii Country Boy.

image
na

Habari10 January 2022 - 04:42

Muhtasari


•Mkataba Kati Ya Konde Music Worldwide Na @countrywizzy-tz Umemalizika Hii Leo Tar 8 January 2022

Harmonize na Country Boy

Msimamizi wa lebo ya Konde Gang msanii Harmonize ametangaza kusitisha uhusiano wa kazi na msanii Country Boy.

Kupitia ukurasa wa instagram wa Konde Gang ilitoa taarifa kwamba wamekubaliana kuacha kufanya kazi na rapa huyo baada ya kumalizika kwa mkataba wa mwanamuziki  huyo ambaye aikuwa amesaini mkataba na lebo hio.

Kwenye taarifa hio walisema kuanzia tarehe 8 januari mwaka huu, Country Boy atakuwa msanii atakayekuwa anajisimamia binafsi kwa kazi za muziki wake. 

"Mkataba Kati Ya Konde Music Worldwide Na @countrywizzy-tz Umemalizika Hii Leo Tar 8 January 2022.Kuanzia Leo Country Wizzy Atakuwa Msanii anaejitegemea Baada Ya Kuafikia Makubaliano Ya Pande Zote Mbili.

Isitoshe, walimtakia mwanamuziki huyo kheri njema katika safari yake ya muziki.

"Konde Music Worldwide Inamtakia Kila Lenye Kheri Country Wizzy Kwenye Career Yake Ya Music Pamoja Na Maisha Kwa Ujumla" 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved