logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Mulamwah bado anamiliki akaunti ya binti yangu-Carol Sonie afunguka kuhusu usimamizi wa akaunti ya binti yake

Watu wengi walibaki wakijiuliza ni nini chanzo cha talaka hiyo lakini yote yaliambulia patupu.

image
na Radio Jambo

Burudani10 January 2022 - 09:40

Muhtasari


  • Miezi kadhaa iliyopita, Mulamwah na mkewe carol Sonie walitengana baada ya kumkaribisha binti yao mzaliwa wa kwanza
  • Watu wengi walibaki wakijiuliza ni nini chanzo cha talaka hiyo lakini yote yaliambulia patupu

Aliyekuwa mpenzi wake chekeshaji Mulamwah,Carol Sonie kwa mara ya kwanza amefunguka kuhusu anayemiliki akuanti ya mitandao ya kijamii ya binti yake.

Miezi kadhaa iliyopita, Mulamwah na mkewe carol Sonie walitengana baada ya kumkaribisha binti yao mzaliwa wa kwanza.

Watu wengi walibaki wakijiuliza ni nini chanzo cha talaka hiyo lakini yote yaliambulia patupu.

Mulamwah alifunguka akisema kuwa baadhi ya mambo ni bora yaachwe bila kusemwa badala ya kusema ni nini chanzo cha talaka na kumuumiza mke wake wa zamani.

Saa kadhaa zilizopita, Carol alichapisha kwenye ukurasa wake rasmi wa Instagram akiwapa wafuasi wake fursa ya kumuuliza swali lolote ambalo wamewahi kutaka kumuuliza.

Mmoja wa wafuasi wake alimuuliza ni nani anayemiliki na kusimamia akaunti ya binti yao ya Facebook kwa vile ingali hai hata baada ya wao kutalikiana.

Carol alijibu akisema kuwa Baba wa bintiye, Mulamwah ndiye anayemiliki na anaidhibiti na hana tatizo na hilo.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved