logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Kambua asimulia unyanyapaa aliopitia baada ya kumpoteza mtoto

Mama huyo wa watoto wawili, anasema kupoteza mtoto hakuathiri mzazi pekee ila  pia familia nzima kwa jumla.

image
na

Burudani11 January 2022 - 05:32

Muhtasari


• Kupoteza mtoto ni mwiko. Nimejifunza hili kutoka kwa ninaowapenda ambao wametembea safari hii .

• Unyanyapaa, aibu, kukosolewa, hukumu, maswali yasiyo na mwisho na ushauri usio na mwisho yote ni mambo aliyokumbana nayo.

Mwanamuziki Kambua

Msanii wa nyimbo za injili Kambua Jumatatu alifunguka kuhusu mambo aliyoyapitia alipoteza mtoto wake wa pili.

Kambua alitumia  ukurusa wake wa Instragram kueleza aliyokumbana nayo wakati alipokuwa akiomboleza  mtoto huyo wake. 

Alisema amekuwa akisoma kitabu ambacho kilikuwa kikiangazia masuala mbalimbali kuhusiana na huzuni iliyojadiliwa na pia kupeana mafunzo kadha kwa kadha.

 Mama huyo wa watoto wawili, anasema kupoteza mtoto hakuathiri mzazi pekee ila  pia familia nzima kwa jumla.

"Kupoteza mtoto hakuathiri mzazi pekee, pia kunaathiri ndugu, babu, bibi, shangazi, marafiki na kila mtu ambaye alikuwa na matumaini ya kukutana na mtoto."  alisema Kambua.

Aliongeza kwamba kupoteza mtoto katka baadhi ya jamii huchukuliwa kama mwiko, huku akikiri aliyopitia kipindi hicho cha kuomboleza mtoto wake.

"Kupoteza mtoto ni mwiko. Nimejifunza hili kupitia watu ninaowapenda ambao wametembea safari hii . Unyanyapaa, aibu, kukosolewa, hukumu, maswali yasiyo na mwisho na ushauri usio na mwisho . Lakini nimejifunza kulinda imani yangu kwa ukali na kwa gharama" yo yoyote ile.”


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved