"Sisi tuliachana kitambo sana hata kabla mtoto azaliwe" Mulamwah asema

Muhtasari

•Ningeomba sana hata kwa mahusiano yake ingine aendelee kuwa mtulivu na mvumilivu.

•Alieleza sababu zilizofanya kuachana na mpenzi wake wa zamani  na kusema kuwa waliachana  wakati Sonie alikuwa na ujauzito wa miezi mitatu, lakini alichagua kukaa kimya hadi pale mtoto alizaliwa 

Mulamwah na Carol Sonie
Mulamwah na Carol Sonie
Image: INSTAGRAM// MULAMWAH

Mcheshi Mulamwah  amejitokeza hadharani kuzungumzia kutengana kwake na mama wa mtoto wake Carrol Sonie.

Mulamwah alikuwa akizungumza na kituo kimoja  cha  radio nchini, alieleza sababu zilizofanya kuachana na mpenzi wake wa zamani  na kusema kuwa waliachana  wakati Sonie alikuwa na ujauzito wa miezi mitatu, lakini alichagua kukaa kimya hadi pale mtoto alipozaliwa.

Aliongeza kwamba mpenzi huyo wake wa zamani hakuwa mvumilivu, kuelewa hali ilivyokuwa wakati huo  kuweza kukidhi baadhi ya matakwa yake ila alianza kuomba usaidizi kwa watu wengine.

"Ningeomba sana hata kwa mahusiano yake ingine aendelee kuwa mtulivu na mvumilivu...hizi vitu zote tutapata. unapata labda kuna wakati singeweza  kukimu  hiki na kile. yeye angeenda kutafuta mahali fulani ama kwa jamaa wake na nilikuwa nakwazika kweli kweli," Mulamwah alisema aliyokuwa akipitia kipindi hicho walichokuwa na Sonie.

Isitoshe hakusahau kuwashauri warembo, "Ningependa kuambia madem watupatie wakati, usiharakishe, utapata hayo matunda yanaendea mwengine,"