• Edday alitangaza anapendekeza rafiki yake wa miaka mingi Julie Mbogo kuwania kiti cha useneta wa Nairobi kuliko Mama wa mtoto wa Samidoh, Karen Nyamu.
Mke wa staa wa Mugithi almaarufu Samidoh, Edday Nderitu ametangaza hadharani anayependelea kuwa seneta wa Nairobi.
Kupitia ukurusa wake wa Instagram, Edday alitangaza anapendekeza rafiki yake wa miaka mingi Julie Mbogo kuwania kiti cha useneta wa Nairobi kuliko Mama wa mtoto wa Samidoh, Karen Nyamu.
Edday Samidoh alichapisha picha ya Julie huku akisema "seneta wangu wa Nairobi"
Mashabiki wake wa mtandao hawakufumbia macho ujumbe wake ambapo walitoa maoni yao huku wakipongeza kwa kusimama na rafiki yake. Baadhi ya maoni yao yalikuwa kama ifuatavyo;
@susankarimi7 Una haki ya kumuunga utakaye. kama kuna mtu hajafurahishwa na hilo aende akaposti mwenye anamuunga kwa ukurasa wake alaa..
@musyoka_musau_ Huyu hawezani na force ya Nyamu wacha aibu ndogo...
@wambomacharia-Jamani! Nampenda Edith ndo huyu seneta wetu kanairo. Huko ukienda nakufuata ooh
Mke wa samidoh aidhinisha BFF kwa kiti sawa na Karen Nyamu.