logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Niko tayari kumzalia Bahati mtoto mwingine Diana B asema

Diana amekuwa kwenye ndoa kwa miaka sita na kuweza kubarikiwa na watoto wawili ambao ni Heaven na Majesty.

image
na

Habari13 January 2022 - 04:22

Muhtasari


• Diana B amejitokeza wazi na kumwambia mumewe,Bahati yuko tayari kumzalia mtoto mwingine.

Bahati na mkewe Diana Marua

Mwanamuziki Diana Marua almaarufu Diana B amejitokeza wazi wazi na kumwambia mumewe, Bahati kwamba yuko tayari kumzalia mtoto mwingine.

Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Diana aliwaambia mashabiki wake kuwa yuko tayari  kupata mimba tena.

Wapenzi hao Diana na Bahati, hivi majuzi wamewajibu wakosoaji wao kuwa watakaa pamoja hadi kifo kiwatenganishe.

Diana amekuwa kwenye ndoa kwa miaka sita na kuweza kubarikiwa na watoto wawili ambao ni Heaven na Majesty.

Rapa huyo alibainisha kuwa anataka kupata mtoto mwingine na kipenzi chake mwaka huu, kulingana naye mayai yake yalikuwa yanacheza, na kumshawishi apate mtoto mwingine.

“Leo usiku itabidi bahati @bahatikenya acheze kama yeye!!! Mwaka huu, nampa mtoto mwingine, mmoja wa mwisho” Alisema Diana.

Diana na Bahati wanajivunia familia yao kwani kila mara huonyesha watoto wao kwenye mitandao ya kijamii.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved