logo

NOW ON AIR

Listen in Live

"Sasa nini imekuua?" Akothee aomboleza mfanyikazi wake aliyefariki ghafla

Rais huyo wa kina mama wasio na waume wa kujitangaza amebaki akishangaa bustani yake na mbwa wake na familia ya marehemu zitachungwa na nani kufuatia msiba huo.

image
na Radio Jambo

Yanayojiri13 January 2022 - 13:58

Muhtasari


•Rais huyo wa kina mama wasio na waume wa kujitangaza amebaki akishangaa bustani yake na mbwa wake na familia ya marehemu zitachungwa na nani kufuatia msiba huo.

Mwanamuziki na mjasiriamali maashuri Esther Akoth almaarufu kama Akothee yuko katika hali ya kuomboleza kufuatia kifo cha ghafla cha mfanyikazi wake mmoja.

Mama huyo wa watoto watano amempoteza mfanyikazi wake ambaye kwa kawaida alihudumia bustani yake na mbwa wake.

Kifo cha mfanyikazi huyo kimempata mwanamuziki huyo kwa mshtuko mkubwa na kumuacha na maswali chungu nzima yasiyojibika.

Rais huyo wa kina mama wasio na waume wa kujitangaza amebaki akishangaa bustani yake na mbwa wake na familia ya marehemu zitachungwa na nani kufuatia msiba huo.

"Kifo cha ghafla cha mfanyakazi wangu mmoja kimeniacha nikijiuliza, inakuwaje mtu aamke akiwa amekufa? Charo sasa nini imekuuaa? Na hii garden umeachia nani wewe? na akina salome? Bibi yako na watoto umeachia nani Charo? Charoooooooo! Charoo jina rahisi katika kinywa changu" Akothee ameomboleza kupitia ukurasa wake wa Instagram.

Wanamitandao wameendelea kumfariji mwanamuziki huyo na kumtakia mfanyikazi huyo wake mapumziko ya amani.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved