logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Sailors Gang yakanusha madai ya Rachel Mwalimu aliyayosema

Sailors  Gang ilitambulika kuwa mojawapo ya wanzilishi  wa mtindo wa aina ya muziki wa Gengetone

image
na

Habari19 January 2022 - 12:53

Muhtasari


•Sailors  Gang ilitambulika kuwa mojawapo ya wanzilishi  wa mtindo wa aina ya muziki wa Gengetone ambao ulipendwa sana hasa na vijana wa kizazi kipya.

•Mwalimu Rachel alikuwa meneja wao ambaye alikuwa anaendesha shughuli zao vizuri  hadi siku ile waligundua kiasi  cha pesa alichokuwa akipata dhidi ya kiasi walichokuwa wakipokea.

Sailors-3-551x600

Mmoja wa kikundi cha sailors gang Lexxy Yung amejitokeza na kupinga kauli ya muigizaji Mwalimu Rachel ambayo alisema si yeye alikuwa chanzo kuu cha kundi hilo kusambaratika.

Sailors  Gang ilitambulika kuwa mojawapo ya wanzilishi  wa mtindo wa aina ya muziki wa Gengetone ambao ulipendwa sana hasa na vijana wa kizazi kipya.

Kupitia ukurusa wa Instagram, Lexxy Yung amekanusha madai ambayo mwigizaji Mwalimu Rachael alisema hivi majuzi kufuatia kile alichoeleza kuwa yeye aliwasaidia kukuza muziki wao na kufanya wajulikane zaidi humu nchini.

Kulingana naye Mwalimu Rachel alikuwa meneja wao ambaye alikuwa anaendesha shughuli zao vizuri  hadi siku ile waligundua kiasi  cha pesa alichokuwa akipata dhidi ya kiasi walichokuwa wakipokea.

"Ninataka watu wajue ukweli wa  kilichokuwa kikiendelea baina yetu na Mwalimu..Mwalimu hatukuwa na muktaba na yeye... ilikuwa tu urafiki. tukamuagiza atusimamie kama Meneja na kweli bila yeye hatungejulikana...lakini yeye kuchukua akaunti zetu  haikuwa jambo nzuri ..alichukua Mdudo,Boomplay,  akachukua skiza, Youtube , twitter na Istagram  na hakutaka kurejesha" alieleza Yung.

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved