logo

NOW ON AIR

Listen in Live

'Mnazuia baraka zangu' Willy Pozee awambia wanaomuita Mkunaji

Kulingana naye wimbo ambao ametoa mwaka huu haufanyi vizuri kwa sababu ya itikadi za jina ambalo mashabiki wake walimbandika.

image
na

Yanayojiri25 January 2022 - 05:18

Muhtasari


• Alipakia video akiwaeleza  mashabiki wake kwamba mwaka huu mpya anawaomba waache kumwita jina hilo

• Sitaki kuitwa bwana mkunaji kwa sababu mnazuia baraka za wimbo mpya wa  toto kutambulika

 

Willy paul

Msanii Wilson Abubakar Radido almaarufu Willy Pozee amelezea kukerwa na wanamitandao wanaomuita Bwana  Mkunaji.

Kupitia ukurasa wake wa Instagram alichapisha video akiwaeleza  mashabiki wake kwamba mwaka huu mpya anawaomba waache kumwita jina hilo.

"Tafadhali, watu wangu, acheni kuniita bwana mkunaji. sitaki kuitwa bwana mkunaji kwa sababu mnazuia baraka za wimbo mpya  wa  toto kutambulika," Willy alieleza.

Hivi majuzi Willy Paul alitoa taarifa akieleza maana fiche ya mkunaji.

,'Mkunaji' ni jina ambalo linahusishwa na mambo mabaya na kudai matatizo mengi  yamekuwa yakimkumba kutokana na jina hilo.

"Ninapenda kuchukua fursa hii kuwafahamisha wote kuwa kuanzia leo sitakuwa natumia jina la 'MKUNAJI', ni baya na sitaki kujihusha nalo! Tangu nilipokubali jina hilo nimekuwa na matatizo mengi sana"alisema Pozee.

Kulingana naye wimbo ambao ametoa mwaka huu haufanyi vizuri kwa sababu ya itikadi za jina ambalo mashabiki wake walimbandika.

  


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved