logo

NOW ON AIR

Listen in Live

BASATA yakutanisha Alikiba, Diamond na Harmonize

Kulingana nao, tuzo hizo zitashirikisha wasanii kutoka ndani ya nchi pekeeTanzania.

image
na

Yanayojiri27 January 2022 - 10:41

Muhtasari


  • BASATA latarajia kukuwakutanisha wasanii sifika wa nchi hio kwenye uzinduzi anaofanyika tarehe 28 Januari 2022
  • Baraza hilo ambalo limekuwa limesitisha tunzo hizo kwa muda limetangaza kupitia ukurasa wao wa instagramu kwamba wanarudisha tunzo hizo
Harmonize,Alikiba na Diamond

Baraza la Sanaa Nchini Tanzania, BASATA latarajia kukuwakutanisha wasanii sifika wa nchi hio kwenye uzinduzi anaofanyika tarehe 28 Januari 2022.

Baraza hilo ambalo limekuwa limesitisha tuzo hizo kwa muda,lilitangaza kupitia ukurasa wake wa instagram kwamba wanarudisha tuzo hizo.

Kulingana nao, tuzo hizo zitashirikisha wasanii kutoka ndani ya nchi pekeeTanzania.

Wasanii  ambao wamepokea mwaliko rasmi ni;Alikiba, Diamond, Harmonize,Nandy, Zuchu na miongoni mwa wengine.

Alikiba anatarajiwa kukaa meza moja na Diamond jambo ambalo si la kawaida kwani  wasanii hao wawili  hawajawai kutana kwenye tamasha yoyote. 

Isitoshe, itakuwa mara  ya kwanza Diamond kukutana na Harmonize baada ya kugura Lebo yake ya WCB na kutengeneza Lebo yake mpya.

Harmonize mwezi jana alipokuwa akirejea nchini Tanzania, alieleza yote yaliyomkumba wakati alikuwa akifanya kazi na Lebo  ya Diamond.

Kilichoshangaza  zaidi kwenye mialiko hio , Diamond na Zuchu ndio wamepokea mwaliko rasmi kutoka timu wasafi.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved