Habari za Zuchu na Diamond Platnumz zimekuwa zikienea kwa kasi, si kwa vyombo habari, si kwa mtandao wanablogu hawajasazwa.
Tetesi za mahusiano baina ya wanamuziki hao zimefanya Mamake Zuchu, Bi Khadija Kopa wiki jana kujitokeza na kuzungumzia mahusiano ya mwanawe na Diamond.
Zuchu alisajiliwa kwenye Lebo ya Wasafi, Aprili 8, 2020, ambapo amekuwa akitamba kwa ngoma kali za Bongo kama vile Sukari, Mwambieni, Nyumba ndogo miongoni mwa vibao vingine.
Wawili hao wamekuwa na ukaribu wenye viulizo si haba hasa baada ya kunaswa hotelini wakiwa wanaburudika pamoja mwezi uliopita.
Bi Khadija alisema mwanawe amelipiwa mahari bila kutaja mtu aliyemlipia.
Kauli hiyo ya Bi Khadija iliwadia baada ya zuchu kuthibitisha kuwa kwenye uhusiano wa kimapenzi na mtu aliyempatia zawadi ya mdoli ya mdoli mkubwa.
“Mimi sina taarifa kwamba anaolewa na Diamond, lakini ninachojua tayari zuchu amelipiwa mahari…”Bi khadija alisema.