logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Akuku Danger ana moyo wa dhahabu-Sandra Dacha asema huku akifichua uhusiano wake na mcheshi huyo

Mwigizaji huyo pia alifichua muda ambao wamekuwa pamoja na sifa maalum

image
na Radio Jambo

Yanayojiri28 January 2022 - 08:34

Muhtasari


  • Mwigizaji huyo pia alifichua muda ambao wamekuwa pamoja na sifa maalum zinazomfanya avutiwe na mchekeshaji huyo

Muigiaji Sandra Dacha anayefahamika sana kama Silprosa kwa mara ya kwanza amewajibu mashabiki wake ambao wamekuwa wakiuliza uhusiano wake na mcheshi Akuku Danger.

Akiwa kwenye mahojiano na mpasho, wakati wa hafla ya kuchangisha pesa za kulipa bili ya mcheshi huyo alisema kwamba ana uhakika kwamba mpenzi wake atarudi nyumbani.

"Akuku is my Bae...he is my boyfriend. Now that he is healed, Kijana anafaa aende nyumbani, akule na akule ndio apone kabisa. Kijana saizi hakuli vizuri. If you gerrit you gerrit," Sandra Dacha alifichua.

Mwigizaji huyo pia alifichua muda ambao wamekuwa pamoja na sifa maalum zinazomfanya avutiwe na mchekeshaji huyo.

"Mwaka mmoja, unajua dawa ya puto ni sindano. Yeye ni aina yangu. Akuku ana moyo wa dhahabu...kisha tabasamu lake...oh Mungu wangu. Ni mtu mzuri," Sandra Dacha alisema.

Harambee iliyofanyika katika Ukumbi wa Kitaifa wa Kenya siku ya Alhamisi ilileta pamoja wacheshi, wasanii na waigizaji.

Katika kikao hicho, wasanii walifanikiwa kukusanya takriban 164,000 ambazo zitatumika kulipia kwa kiasi bili ya hospitali ya Ksh 1 Milioni.

Sandra alisema michango hiyo itaendelea hadi Akuku Danger atakapofanikiwa kurudi nyumbani.

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved