logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Mchekeshaji Akuku Danger alazwa hospitalini tena kufuatia matatizo ya kupumua

Mwigizaji Sandra Dacha amefichua kwamba Akuku amelazwa katika chumba maalum cha wagonjwa cha HDU

image
na Radio Jambo

Yanayojiri31 January 2022 - 06:16

Muhtasari


•Mwigizaji Sandra Dacha amefichua kwamba Akuku amelazwa katika chumba maalum cha wagonjwa cha HDU.

Mchekeshaji Akuku Danger alazwa tena siku chache tu baada ya kuruhusiwa kutoka hospitalini

Siku chache tu baada ya kuruhusiwa kutoka hospitali, mchekeshaji wa Churchill Show Akuku Danger amelazwa tena.

Kupitia ukurasa wake wa Instagram, mwigizaji Sandra Dacha almaarufu kama Silprosa amefichua kwamba Akuku amelazwa katika chumba maalum cha wagonjwa cha HDU.

Dacha ameeleza kwamba mchekeshaji huyo alilazwa Jumapili baada ya kuathiriwa tena na matatizo ya kupumua.

"Tumerudi hospitalini tena. Matatizo ya kupumua tena. Yuko katika HDU tunapozungumza. Endeleeni kumwombea Akuku Danger" Dacha alitangaza.

Akuku Danger aliruhusiwa kwenda nyumbani wiki iliyopita baada ya kuwa amelazwa kwa kipindi cha wiki kadhaa.

Mchekeshaji huyo alilazwa katika hospitali ya Nairobi mwishoni mwa mwaka jana baada ya kushambuliwa na ugonjwa wa Pneumonia.

Dacha ambaye hivi majuzi aliweka wazi mahusiano kati yake na mchekeshaji huyo amewasihi Wakenya kuendelea kumwombea mpenzi wake apate afueni.

"Endelea kupambana mpenzi!" Dacha amemtia moyo Akuku Danger.

Mamia ya wanamitandao wameendelea kumtakia Akuku Danger afueni ya haraka.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved