logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Tuanze na Collabo gani? Nandy awauliza Mashabiki

Nandy ametoa orodha ya wasanii ambao amefanya Collabo nao huku akitaka mashabiki  wamshauri ni Collabo gani  wangetaka kusikia ikiwa ya kwanza kutoka kwa Orodha hiyo.

image
na

Yanayojiri01 February 2022 - 10:49

Muhtasari


• Msanii wa Tanzania Nandy almaarufu The African Princess amejitokeza na kuwauliza mashabiki wake wamshauri kuhusu  msanii wa kwanza ambaye wangependa afanye naye collabo.

• Baadhi ya wasanii aliowataja kwenye orodha ya hiyo ni; Sauti Sol, Patoranking, Davido na dulamakabila.

 

 

Nandy the African princess

Msanii wa Tanzania Nandy almaarufu The African Princess amejitokeza na kuwauliza mashabiki wake wamshauri kuhusu  msanii wa kwanza ambaye wangependa afanye naye collabo.

Kupitia ukurusa wake wa Instagram, Nandy ametoa orodha ya wasanii ambao anatarajia kuingia nao studio kuandaa muziki huku akitaka mashabiki  wamshauri ni Collabo gani  wangetaka kusikia kwanza.

Baadhi ya wasanii aliowataja kwenye orodha hiyo ni; Sauti Sol, Patoranking, Davido na dulamakabila. 

Vilevile, ameeleza kuwa collabo hizo ziko tayari kilichosubiriwa ni mashabiki kusema wimbo gani wanataka awapakulie mwaka mpya.

Nandy ambaye pia  ni muigizaji wa filamu Tanzania, amekisiwa kwamba  mwaka huu wa 2022atafunga ndoa siku za hivi karibuni kumekuwa na tetesi mwaka huu 2022 lazima atafunga ndoa na mpenzi wake Bilnass.

Jumatatu, msanii huyo alitangaza kuwa anaendelea na vikao vya kupanga mikakati ya tamasha lake ambalo linatabiriwa kufanyika kabla mwezi wa nne ,huku mipango kabambe ikishika kasi kuhakikisha kila kitu kinashughulikiwa kabla ya tarehe rasmi.

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved