logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Mercy Masika awashauri vijana kutocheza ngoma za unyumba kabla ya ndoa

Kupitia video aliyopakia kwenye ukurasa wake wa instagram  alieleza vijana kuwa ni vizuri kuepuka tendo la ndoa wakati hawapo tayari kutulia  kuwa na familia.

image
na

Makala04 February 2022 - 10:56

Muhtasari


• Mwanamuziki, Mercy Masika amewarai  vijana ambao bado hawajafunga ndoa kujitenga na ngoma ya ndoa hadi watakapo ingia katika ndoa.

• Alieleza vijana kuwa popote watapokuwa  wakitembea  watakutana na watu  wanaovutia zaidi hivyo basi hio isiwe ni kizingizio cha kujamiana kiholela.

Msanii wa injili, Mercy Masika

Mwanamuziki, Mercy Masika amewarai  vijana ambao bado hawajafunga ndoa kujitenga na ngoma ya ndoa hadi watakapo ingia katika ndoa.

Kupitia video aliyopakia kwenye ukurasa wake wa instagram  aliwashauri vijana kuwa ni vyema vizuri kuepukana na tendo la unyumba na ilhali hawako tayari kuanza familia.

Alieleza vijana kuwa popote watapokuwa  wakitembea  watakutana na watu  wanaovutia zaidi hivyo basi hio isiwe ni kizingizio cha kujamiana kiholela.

"Siku zote utapata watu wa kuvutia popote uendapo iwe umeoa au hujaolewa. Watu wa kuvutia watakuwepo kila wakati," alisema Mercy masika.

Isitoshe, alizungumza kuhusu wanandoa ambapo aliwashauri kuwa wajasiri na wavumilivu kwenye ndoa kwani anaelewa vyema ndoa sio jambo rahisi hasa  wakati huu wa karne ya ishirini na moja.

"Kuwa hodari na jasiri kwenye ndoa ni kukubali kuwa wewe ni mzuri...kuwa hodari katika maisha kama Mungu anavyotaka kutoka kwako," alieleza. 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved