logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Baadhi ya 'scandals' ni sisi wasanii utengeneza,'Willy Paul asema huku akiahidi mashabiki wake haya

Hii ni moja wapo ya mbinu ambayo wasanii wengi hutumia katiika karne hii ya sasa.

image
na Radio Jambo

Yanayojiri05 February 2022 - 21:08

Muhtasari


  • Wasanii wengi wanafahamika kutafuta kiki ili kibao chao kipya kiweze kuvuma na kupokea watazamji weni kwenye Youtube

Msanii Willy Paul alifahamika sana baada ya kujitosa kwenye tasnia ya muziki, miaka 5 iliyopita, huku akifahamika sana mitandaoni kupitia kwa nyimbo zake.

Safari ya muziki ya msanii huyo haijakuwa rahisi kwani amekuwa akipokea kejeli mitandaoni, hii ni baada ya kuacha kuimba nyimbo za injili.

Licha ya hayo yote msanii huyo amekuwa akitia bidii kila kuchao, ili kuhakikisha mashabiki wake wameburudika.

Kupitia kwenye ukurasa wake wa instagram aliwaahidi mashabiki wake muziki mzuri mwaka huu, huku akidai kwamba baadi ya kashfa ambazo mashabiki uhuhudia mitandaoni ni wasanii huwa wanatengeneza wenyewe.

Wasanii wengi wanafahamika kutafuta kiki ili kibao chao kipya kiweze kuvuma na kupokea watazamji weni kwenye Youtube.

Hii ni moja wapo ya mbinu ambayo wasanii wengi hutumia katiika karne hii ya sasa.

"Hello fam, more music less scandals. Btw some of the scandals you see out there.. ni sisi wasanii utengeneza but this year expect nothing but good music..." Pozze Aliandika.

Kulingana na maoni yako je wasanii wanapaswa kutafuta kiki kwa ajili ya vibao vyao?


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved